Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiongozwa na Spika wa Bunge la Burundi,Pie Ntavyohanyuma baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Bujumbura, ambako leo atamwakilisha Rais Jakaya Kikwete katika sherehe za kumwapisha Rais wa Nchi hiyo, Pierre Nkurunzinza.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwapungia wananchi wa Burundi waliofika kwenye uwanja wa ndege Bujumbura, ambako leo atamwakilisha Rais Jakaya Kikwete katika sherehe za kumwapisha Rais wa Burundi, Pierre Nkurnzinza. Kulia ni Spika wa Bunge la Nchi hiyo Pie Ntavyohanyuma na wapili kushoto ni mkewe Tunu.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na watanzania waishio Burundi baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Bujumbura ambako leo atamwakilisha Rais Jakaya Kikwete katika sherehe za kuapishwa kwa rais wan chi hiyo, Pierre Nkurunzinza.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na mkewe Tunu wakizungumza na Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maziwa Makuu, Balozi Liberat Mulamula (kulia) baada ya kuwasili jijini Bujumbra, ambapo leo atamwakilisha Rais Jakaya Kikwete katika sherehe za kumwapisha , Rais wa Burundi Pierre Nkurunzinz.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 13 mpaka sasa

  1. Kulikoni huyo Bw nyuma ya Pinda kny Red carpet ana brifcase tena kny parade, au ndio protocal?

    ReplyDelete
  2. Speaker ana shape nzuri ya kupanda juu sana! Safi kweli. Kila la kheri Mheshimiwa Pinda. Rais mtarajiwa 2015

    ReplyDelete
  3. Mkuu Pinda na mywife wako mko juu sana yani wamependeza mpaka raha

    ReplyDelete
  4. Kwa nini JK hajaenda? Anaumwa?

    ReplyDelete
  5. Hebu tuambieni Balozi wetu Bujumbura hayupo ama vipi? Picha zote haonekani.

    ReplyDelete
  6. Godfather: 05:46:00 PM, yaonekana kama angekwenda ungezusha swali, "Vasco da Gama" hawezi kuwaachia wengine wamwakilishe?

    ReplyDelete
  7. Tai ya Pinda ni ya muongo upiiiiiii(1970's, 80's 90's au 2000's)!? Mnaojua trend ya tai tayari mna jibu.

    ReplyDelete
  8. Naona Pinda anawapiga watu na kumi.

    ReplyDelete
  9. mie nilihani anasema "don't touch me"....kumbe anapungia mikono...au ni macho yangu

    ReplyDelete
  10. nakubaliana na mshangiaji wa pili?

    ReplyDelete
  11. Jamani watu wa PR wardrobe department inabidi mumshauri Waziri mkuu utaratibu wa Suti. Ukiwa umesimama au unatembea unafunga vifungo na ukikaa ndio unafungua ili uwe comfortable na pia vifungo visije achia.
    Haya ni mambo ya kawaida na utaona mtu akisimama tu anafunga na akikaa anafungua. Sasa namna hii anakuwa kama Don au mwanamuziki ambako kila mtu anajiainisha kivyake.

    Ni kazi yenu kumshauri sio mnajaza tu per diem!!
    Mzawa

    ReplyDelete
  12. godfather: yuko ktk kampeni sasa ya kutujulisha anaingia awamu ya 2 ya miaka 5

    ReplyDelete
  13. Wewe: Tai ya Pinda ni ya muongo upiiiiiii(1970's, 80's 90's au 2000's)!? Mnaojua trend ya tai tayari mna jibu.

    Sisi hatuvitengenezi hivyo vya kisasa kuweza kukidhi mahitaji ya kukogana kila siku; ndio maana hatuendelei!

    Na wewe: Fri Aug 27, 08:21:00 AM. Wengine hatuoni cha maana na hayo uliyoshauri.

    Hiyo tai ni swafi sana>

    FASHIONISTA MWENYEWE

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...