Ankal,

Pole kwa kazi.
Hivi karibuni nilisafiri kutoka Bukoba kuja Mwanza kwa MV Victoria. Kilichonishangaza ni wahusika melini kutozingatia umuhimu wa kuacha wazi eneo kunakohifadhiwa "life jackets" kama ilani inavyoelekeza. Ikitokea ajali (Mungu apishie mbali) mpaka mizigo ihamishwe ndo mlango wa life jackets ufunguliwe!
Nawasilisha.

Makame

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 22 mpaka sasa

  1. Katika hili sii mara ya kwanza kuliona ndani ya meli hiyo ya MV Victoria. Tenahapo mizigo haikuwa mingi. Mara nyingi hujazwa ndizi hadi kule juu sehemu ya kupandia Life boats. Tena eneo hilo ni pembezoni mwa quaters za mabaharia na nikaribu kabisa na chumba cha Nahodha Capt Mwasa kama bado atakuwa anacomand meli hiyo. Ni vyema watu wa sumatra wakawa na kaguzi za mara kwa mara nyakati hizi maana sidhani kama watu woote wanaopanda chomboni wanakuwa na tahadhari ya hali gani?
    Tunakushukuru sana mdau kwa kutuelimisha na kutupa taswira halisi

    ReplyDelete
  2. ACHA UNOKO, ILI WATU WASIWEKE MIZIGO WAKOSE NAULI ZA MIZIGO, ACHA KUFUATILIA KAZI ZA WATU

    ReplyDelete
  3. Anony wa pili yaonekana unamazowea ya kusafiri kwa punda ama baiskeli. Hujawahi kupanda melini ukakutana na dhoruba. Huo sii unoko wala kufuatilia kazi za watu ni suala la tahadhari tu!

    ReplyDelete
  4. ajali haina kinga banaaa!!!!

    ReplyDelete
  5. NYIE MNASHANGAA NINI SASA HEBU NENDENI MV MAGOGONI NA MV KIGAMBONI MJIONEE LIFE JACKETIS ZIMEFUNGIWA NA VIRO,SOLEX HADI KUFURI ZIMESHIKA KUTU.SINA KAMERA NINGEWALETEA PICHA ,KAMA YUPO MWENYE KAMERA AKAPIGE HATA SASA.SIKU AJALI IKITOKEA NI YALE YALEEEEEEEE

    ReplyDelete
  6. mimi kaka misoup ndizi hizo tu mimi hoi na miss kweli kweli, Nshamba kwetu

    ReplyDelete
  7. Huyo Anony no 2. Nenda kanunue kitabu "Sitasahau MV Bukoba" Ndio utajua ukiwa makini, ajali inakingika. Tunasubiri mpaka watu wafe ndio mamlaka husika ianze kusema meli ilijaza kupita kiasi.

    ReplyDelete
  8. KINGA IPO UKICHUKUA TAADHALI

    ReplyDelete
  9. Anon wa pili na wa nne nyie kweli ndo wale wajinga wajinga hamjali maisha na usalama wa watu.Eti ajali haina kinga,mtaendelea kufa kijinga jinga sababu ya mentality kama zenu.Anon wa pili hujawahi sikia tahadhari yakinga ajali? Watu wengine kweli ni mambumbu.Kama ajali haina kinga mbona unasubiri magari yapite ndipo uvuke barabara?

    ReplyDelete
  10. nadhani hamna haja ya kubishana na anony wa pili,sababu nimegundua kwamba hata life jacket hajui ni nini,na inakazi gani,so mtu wa hivyo mtabishana mpaka asubui,sidhani hata kama anakumbuka issue ya mv bukoba tulivyopoteza wapendwa wetu,yes kifo hakiepukiki lakini lazima tuweke tahadhari,tusikae kusema tu mungu atasaidia,tukumbuke usemi kwamba JISAIDIE NAMI NITAKUSAIDIA.the thing is tahadhari imetolewa na wahusika sababu ni watu wenye akili zao ujumbe wataupata na wataufanyia kazi,keep it up mr,michuzi blog yako inatupa mambo mazuri.BIG UP MEN!!!

    ReplyDelete
  11. why I bother you never publish my comment!!!

    ReplyDelete
  12. anoni (2) na (4) mna vichwa??
    ndani ya vijichwa vyenu kuna kitu?? basi kama huna la kusema si ukae kimya tuuuuu??
    kakulazimisha nani kuandika uchafu??
    tumieni akili zenu.

    ReplyDelete
  13. Ajali ikitokea watu wengi watakufa shauri ya kukosa life jackets! Jamani, hii si mchezo, wenye meli wapigwe faini kali kusudi iwe fundisho. Pesa za haraka au maisha ya mtu nini ina thamani zaidi?

    ReplyDelete
  14. kuna mijitu ya ajabu inapenda kutoa comment kukamilisha ujinga wao.


    yani mtu na akili zako timamu huwezi kuona umuhimu wa hii post?

    ReplyDelete
  15. iki ni kitu cha kusikitisha naona hatujajifunza chochote baada ya ajali ya MV Bukoba including Nahodha wa meli ya Victoria ambaye anapaswa kuchukulia maisha ya abiria wake seriously. Tanzania hatutabadilika mpaka hapo tutakapoelimika kujua haki zetu asilimia yetu kubwa tunafikiria haki inanunuliwa.

    ReplyDelete
  16. NINA MSHUKURU SANA HUYU ALIYETULETEA HIZI PICHA. I HOPE WAHUSIKA WATA LISHUHULIKIA HILI JAMBO. HII NDIO SABABU AJALI ZETU HU UWA WATU WENGI KWASABABU YA UZEMBE KAMA HUU. WALE WENYE KUTOA COMMENTS ZA KUONA HILI JAMBO NI SAWA NINAFIKIRI WANATOA HIZO COMMENTS ILI WAKASIRISHA WATU. MY DEAR THIS IS NOT FUNNY.

    ReplyDelete
  17. Najua michuzi utaibana tu hii! Ila ukweli lazima usemwe na utasemwa tu!

    Hapa ajali ikitokea na watu wakashindwa kuingia na kuchukua hayo maboya ya usalama, na wakafa.
    Tutasema wametolewa kafara! Au upepo mbaya sana ulipita pale! Au watu wamechukuliwa na majini! Au....
    Watanzania sijui lini tutaamka na kujua sasa ndio wakati wa kua na heath and safety na sio kusema eti "ajali haina kina banaa!"
    Tatizo letu ni elimu na kuchukulia mambo kienyeji enyeji tu!
    Na ndio jibu la umaskini wetu!
    Na ndio maana hata CCM hawana wasiwasi, wanajua pamoja na ufisadi, ufujaji wa mali ya umma na kutokuwajibika, bado tu tutawachagua!

    ReplyDelete
  18. Mimi Hapa Nakuja na Solution Tatu!!
    1. Tuna haki ya kuwaponda hawa wasioelewa na kusema ajali haina kinga sijui ulaji hawa ndio ni watovu wa Mawazo na Hawastahili katika Jamii yenye kuhitaji mabadiliko ila wanaowapond pia watoe mawazo yao juu ya mada sio mtu anakuja kuponda tu!!

    2. Wenye mizigo wawajibishwe na wahudumu wa meli ikiwa ni pamoja na faini au kutaifishwa mizogo yote inayokutwa eneo hilo hii ingewastua hata wale wanaojifanya kutia pamba masikio yao!!

    3. Kama wahudumu wa meli wanashondwa kuwawajibishwa hawa wazembe wachache basi wao wawajibishwe na mamlaka husika (sumatra)Ikiwa ni pamoja na faini au kuachishwa kazi kabisa.

    ahsanteni.

    ReplyDelete
  19. Halafu meli ikibinafsishwa na mwenye meli akiajili wakenya, hawa wazalendo watakaofukuzwa kazi kwa kuufumbia macho uzembe huu wataanza kulalamika kwamba "ooh... kwanini wanaajiri wakenya". Wakati ni dhahiri kwamba uwajibikaji unawashinda.

    ReplyDelete
  20. Ninachopenda kusema ni kwamba kuna kitu kimoja ambacho nadhani watu wengi wanshindwa kuelewa, kwamba hakuna ethics in work place, hakuna msisitizo wa ethics mhalia popote kwenye mafunzo. Sasa unatarajia nani atamkaguwa nani, nani atamlipa nani kma akyna ajali, wakati nahodha ni mtoto wa ??????. Na kingine hakuna shirika la uma linafuta ethics za kazi, kama kungekuwa na hilo tungekuwa na umeme kila siku, tungekuwa na maji kila kitongoji, wezi wangekuwa jela na siyo majumbani. Majambazi ndiyo wanioendesha miji, hakuna haki kwa wananchi. Ni saa ngapi mtu atajali kwamba anabiria na ni muhimu kuwatunza vyema na kuwaheshimu. Michuzi usibanie hii. Watu wengi tunanyanyasika kila kona tunahitaji msaada lakini wengine tutakufa hata haki hatutaziona. Mungi ibariki nchi yetu tuangalie sisi walala hoi labda kuna siku mtu atasimama na kusema imetosha tunahitaji kizazi chenye mwelekeo.

    ReplyDelete
  21. na wakenya twanazidi kumiminika tanzania yenu,,,nyie ngojeni tutawafunza adabu na kazi kisawa tu

    ReplyDelete
  22. lol iyo miche ya miti ni mizuri sana made in BK

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...