Michuano ya kusaka nafasi kucheza kombe la dunia mwaka 2010 imeanza leo katika jiji la Pretoria NCHINI AFRIKA KUSINI ambapo TANZANIA imeanza vyema mashindano hayo kwa kushinda mechi yake kwa kwanza kwa magoli 50 kwa 25 dhidi ya Lesotho.
TANZANIA ilionyesha kiwango kizuri katika mashindano hayo kutokanana kucheza mchezo wenye ujuzi mkubwa ambapo iliweza kuisambaratisha LESOTHO .
Akifungua mashindano hayo naibu waziri wa michezo wa AFRIKA KUSINI GERT OOSHIZEN amesema kuwa mashindano hayo yanaimarisha mchezo huo na kuweka ushuaino mzuri baina ya nchi zinazoshiriki.
Mchezo mwingine ulikuwa kati ya ZIMBABWE na AFRIKA kusini ambapo timu hizo zimeonyeshana kazi kubwa kutokana na kila timu kujiandaa vilivyo ambapo AFRIKA KUSINI iliibuka mshindi kwa magoli 64 kwa 29.
Kwa upande wake kocha wa TANZANIA SIMONE MCKIWIS amesema a mefuahia ushindi wa timu yake na kuanhidi watanzania kuwa timu hiyo itaendeela kufanya katika michezo yake inayoendeela ambapo amewataka watanzania kuiunga mkono timu hiyo.
Hata hivyo mashindano hayo yamekosa msisimko mkubwa kutokana na mashabiki wachache kuhudhuria, tofauti na mashindano ya kimataifa yaliyofanyika nchini mwaka jana ambapo watu mbali mbali waliweza kuhudhuria.
Mashindano hayo yanashirikisha timu sita kutoka AFRIKA ambazo ni NAMIBIA,TANZANIA,BOTSWANA,LESOTHO,ZIMBABWE, na wenyeji AFRIKA KUSINI.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. mashindano hayo ni ya mchezo gani?mbona habari haijaeleeza vizuri?

    ReplyDelete
  2. kwani huoni si mashindano ya kupanga mstari,watakaoonyoosha ndio washindi

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...