Gari aina ya Subaru lenye namba za usajiri T 193 AZL ikiwa katika hali mbaya sana mara baada ya kupata ajali jioni hii maeneo ya Kinondoni,Ubalozi wa Ufaransa.gari hii ambayo ilikuwa ikitokea maeneo ya Kinondoni Morocco kuelekea mjini,ilipoteza muelekeo mara baada ya gari moja kuingia ghafla katika barabara kubwa huku gari hii ikiwa katika mwendo wa kasi sana na kumfanya dereva wa gari hii kushindwa kuikontroo gari hii na kwenya kugonga moja ya nguzo za taa za barabarani na kuifanya ikapinduka.ndani ya gari hii kulikuwemo na watu watatu ambao wawili walijeruhiwa na kukimbizwa hospital na mwingine kufanikiwa kutoka bila jeraha lolote.
Sehemu iliyokuwepo nguzo ya taa za barabarani iliyogongwa na gari hiyo na kuifanya ikang'oka kabisa katika sehemu yake.
Mmoja wa waliokuwemo ndani ya gari hiyo (anaetumia simu) ambaye hakutaka kutaja jina lake akijaribu kuwasiliana na ndugu na jamaa kuhusiana na ajali hiyo iliyowakuta leo.
Askari wa Usalama barabarani,akipata maenezo mafupi toka kwa mashuhuda wa ajali hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 12 mpaka sasa

  1. BONGO TUNA STREET RACING SIKUHIZI, UNAWAPATIA VIJANA WA "LAU" KITU GIDOGO TU UNA RACE TARTIBU.

    ReplyDelete
  2. Hivi mtu mzima na akili zake anaposema ajali mbaya sana, je kuna ajali nzuri?

    ReplyDelete
  3. Hiyo ni Subaru ama Impreza au Forester ambayo kwa muonekano wake tu inaonyesha ina turbo na kwa kuwa Subaru ni gari zenye umaarufu wa kukimbia sana na kwa uelewaq duni wa vijana wa kitanzania itakuwa alikuwa mwendo kasi sana bila kuwa na tahadhari na kona zilizopo hapo,la kushukuru ni kwa sasa tunatakiwa kuwa na madereba werevu nao ni wale watakaopata leseni zilizotolewa hivi karibuni kwani hutapata leseni hiyo mpaka uwe TIN,vyeti vya uhalali wa kumiliki leseni na leseni yako ndio upate hiyo leseni mpya,hongera vyombo vya dola (TRA na Polisi) kufikisha hili kwani wahindi na watoto wa mabosi hawatakuwa na upumbavu huu.

    ReplyDelete
  4. Dogo leo jamba jamba kama ndo uliiba gani home cha moto utakiona! Hila pole sana kaka. Hila mzee wa kiswahili hajui hilo lazima fimbo uchezee , wazee badala ya kushukuru dogo mzima wanata muwasha vibao !!lol

    ReplyDelete
  5. mtoa maoni Tarehe Sun Oct 03, 10:03:00 AM, ubaguzi umekujaa mshenzi weee maana jambo dogo tu wahindi... inavyoonyesha walikufanyia kazi na baadae wakakuacha tu maana una chuki nao.. lakini utabaki na chuki zao wenzako watakuachia vumbi...

    ReplyDelete
  6. usizungumzia ubaguzzi kwa taarifa yako hizo leseni wewe utasota kuzipata lakini muhindi ataipata hiyo tin na leseni amekaa nyumbani anakula anaangalia tv

    ReplyDelete
  7. Huyu jamaa tulikuwa nae kwenye maonesho ya magari pale sayansi viwanjani. akanonesha mbwembwe kidogo halafu akaondoka kwa spidi.
    mimi nahisi alikuwa anashindana na magari mengine aliyotoka nayo pale.

    ukiwa na gari inayokimbia sio maana yake uikimbize barabara zetu ni za kila mtu tunataka usalama. wakipona wote tia ndani. na hio gari ndio asahau tena hapo, insurance wamlipe corolla au swift awe na adabu.
    A

    ReplyDelete
  8. Nayachukia sana hayo mabreak down ya bongo ni mabayaa, yanaharibu magari ya watu ikitokea ajali tu yanakuja kumi kwa wakati mmoja, badala ya gari la wagonjwa huu ni upuuzi ati wanawahi kazi, defender za mapolisi ndo yanabebea majeruhi, Mungu jalia nipate hela niwekeze kwenye hiki kitengo cha break down na magari ya wagonjwa.

    ReplyDelete
  9. Huyo kijana 'aliyetoka mzima' namshauri aende hospitali haraka akafanyiwe thorough check-up. Kuumia sio lazima upate jeraha lenye kuvuja damu. Possibility ya internal injuries ipo, na anaweza kuhatarisha maisha yake akidhani hajaumia.


    Karani wa Zahanati
    Ukerewe

    ReplyDelete
  10. Mtoa Maoni Tarehe Sun Oct 03, 10:11:00 PM, bado nitasema mbaguzi. Ikiwa kama mhindi leseni anaipata kakaa nyumbai basi mtoa leseni ni nani? Si mhindi mwenzake lakini ni waswahili walio katika position ya kutoa leseni kwa kitu kidogo. Sasa wa kulaumiwa ni nani hapo? hata kama kuna rushwa basi ni hata mswahili mwenye pesa basi anapata hiyo leseni wakati kakaa nyumbani - sasa kama hapo utazungumzia nini? ukiwa na pesa zako tu basi unapata hii leseni - acha ubaguzi kajinyonge kama una tatizo na wahindi

    ReplyDelete
  11. yaani hili tatizo la ajali sana sana ni wakati week end na usiku limekuwa sugu sana,na pia uendeshaji wa magari kwa usiku ni vurugu sana,ukiangalia hizi barabara watu wanvyoendesha usiku wengine wameshaongeza speed vichwa vyao,na ukija kwa huku mjini hawa ndugu zetu wa asili ya ki asia ndio tabu tupu kwa uendeshaji wa kasi zaidi@daniel

    ReplyDelete
  12. Car racing imeingia bongo bwana, kama uamini pita wakati wa usiku mwingi mitaa ya upanga na mjini kati uone vijana wanavyofanya vitu vyao.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...