JK akihutubia maelfu ya wananchi na wana CCM wa Zanzibar katika uwanja wa Demokrasia (zamani kibanda maiti) huko Unguja jana
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dr. Amani Abeid Karume akipiga chapuo kwenye mkutano huo wa kampeni wa JK katika uwanja wa Demokrasia, Unguja

Waangalizi huru wa uchaguzi wa TEMCO walikuwepo kibao
Waangalizi wa kimataifa, akiwemo ankal Paschal Mayalla, na wenzake pia walikuwapo
Kikosi kazi cha Zenj FM kilikuwepo kurusha laivu tukio hili
wana TEMCO kibao wakiwa bize
Nyomi uwanja wa Demokrasia, Unguja, jana
Uwanja wa Demokrasia ulikuwa mdogo jana...
wana CCM kibao mkutanoni hapo
Mh. Temba na Chegge wa TMK Family walikuwepo kumtambulisha JK kwa wananchi
Marlaw naye akipiga honi kwa wapinzani
Barbara na Lilian walikuwepo pia
Msanii aliye juu kabisa visiwani kwa sasa akitumbuiza
CCM oye!
Mdau wa CCM
wana CCM wa skuta wakimsubiri JK akitokea Pemba JK akiaga uwanja wa Pemba
JK akisalimiana na mgombea ubunge jimbo la Wawi Mh. Daudi uwanja wa Pemba
Ankal akiwa Pemba na m gombea ubunge wa CCM wa jimbo la Mkoani Issa Mohamed Salim (kati) na mgombea uwakilishi wa jimbo la Mkanyageni Masoud Mohamed Abdallah



















Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 16 mpaka sasa

  1. Wana-CCM na Watanzania wenzangu, natoa wito kwenu wote katika kila pembe ya nchi hii, tuongeze juhudi ya jasho, hali na mali katika kampeni hadi siku ya uchaguzi ili tuhakikishe kuwa CCM kinapata ushindi mkubwa sana. What is at stake ni kuwa, kwa mara nyingine tena, CCM imeonyesha kuwa CCM ndicho chama pekee kinachowaunganisha Watanzania wa makabila, dini na rangi zote. Mungu ibariki Tanzania na utudumishie amani. Amen. Sosthenes wa Tabata.

    ReplyDelete
  2. ndo hivyo tu? uncle lakini unajitahidi kumnadi Jk ila hauziki tena. anyway tutawatosa tu mwaka huu,mbona tushawachoka kabla hata ya kampeni!!!!!!!!

    ReplyDelete
  3. jk anauzika sana wewe tu na roho mbaya yako na ccm hatujaichoka wembe ni ule ule ushindi

    ReplyDelete
  4. Wana wa vyama vya upinzani hawajuikupiga hesabu. Ili CCM ing'oke ikulu unganeni kwanza tofauti na hapo mtaisikia tu ikulu. Vijijini hamjapateka vya kutosha wala msidanganyike kuwa watanzania wa leo si wa juzi ulongo. wa tz ni walewale. haki zenu kibao hamzijui nenda dsm utapata jibu kupiga kelele si kujua mambo mengi. Watu wengi wa mjini hamjui mambo mengi ya msingi.Ccm itashinda even at a minimal margin what matters ni white house and Mps and House of Reps. Thanks.

    ReplyDelete
  5. Mmmh!

    Bradha huyo Mdau wa CCM aliyejiandika "CCM" kwenye paji la uso MIDOMO yake nimeipenda imekaa fresh! Daa!

    Ulifanikiwa kupata kontakts zake?

    ReplyDelete
  6. YANI WE MITHUPU UTUZIMA WOTE UHUNI WA JUGNUNERO UJACHA YANI PICHA ZATE UMEONA HIYO NDIO UTIE CCM OYEE TUSHAKUFAHAMU NA UKIFANYA MASIHARA BARA WEYE HURUDI UTANATA VISIWANA USHAFAHAMU

    ReplyDelete
  7. Hivi ni mara ya ngapi Mh Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anakanyaga ZENJI? naombwa kukumbushwa kidogo.Haya AKISHINDA CCM AU CUF zanzibar tushajua tu kuwa vyama vyote vinatawala hakuna wasi wasi na mawaziri wanatoka kote kote ZANZIBAR NI NJEMA SASA MUNGU AWAPE HEKIMA HAO CCM TU WAKUBALI MATOKEO! maana hawajawahi kushinda hata mara moja!

    ReplyDelete
  8. We mchangiaji mada wa pili, nadhani unaishi "Cuckoland". JK na CCM watapata ushindi mkubwa sana come October 31st. Nyinyi kyadema mtalia machozi makavu!!!!

    ReplyDelete
  9. Safari hii CCM kwa mara ya kwanza itashinda Zanzibar na Pemba kihalali.

    ReplyDelete
  10. Sosthenes (anon wa kwanza), nakubaliana na wewe kuwa CCM ndicho chama pekee kinachowaunganisha Watanzania wa makabila dini na rangi zetu. Hapa Sinza kanisani kwetu (nitaminya jina) kumetokea mpasuko baada ya waumini kukataa shinikizo la baadhi viongozi wetu wa kanisa na baadhi ya waumini wenzetu wa kabila fulani kutoka mkoa fulani wa kaskazini la kutaka eti tuwapigie kura watu wa dini yetu. Tuliwaambia waziwazi kuwa tukianza mchezo huo basi sisi kama taifa tutaishia pabaya sana na ahadi ya ufalme wa maziwa na asali itaishia kuwa ndoto ya jinamizi la majonzi. Nawaomba Watanzania wenzangu wote tuwapuuze na tusiwafuate viongozi wa dini wanaosukumwa na chuki ili wasituingize katika majanga makubwa. Ijapokuwa mimi niko NCCR, nitawapigia candidates wa CCM kura kwa kuwa sitaki dini yangu itumike vibaya na kuliangamiza taifa letu. Ewe Mungu wetu tunakuomba ilinde Tanzania yetu. Amen.

    ReplyDelete
  11. halafu wewe ankal dizaini nyoka wewe!

    ReplyDelete
  12. Anon ulinayeongelea kuwa CCM inawaunganisha watu wa dini zote na makabila siyo kweli, napinga na wewe kwa hilo. Wewe ni CCM na wala usisingizie kuwa wewe ni NCCR...hakuna ukweli wowote kuwa CCM inaunganisha watu wa dini na makabila, huu ni utamaduni wetu wa kuwa pamoja na siyo CCM.

    ReplyDelete
  13. TATIZO LA WATANZANIA WANAWAACHIA WALALA HOI KUCHAGUA VIONGOZI, WALALA HOI WA MLO MMOJA, WAKIHONGWA KANGA, CHAKULA, BUKU, BUKU TENI, UKIONA UNAWATOTO WANAKULA UNAFANYA MAMBO YAKO SAAFI, BASI KWAO SAAFI HAWAPIGI MAHESABU YA MIAKA MITANO IJAYO KUTAKUWAJE, SASA NYIE WASOMI NYIE, WENYE PESA ZENU MNAPIGAGA KURA? SI MNASEMA TUKAPIGE TUMCHAGUE NANI SI NDIVYO MNAVOSEMAGA SASA ANGALIENI NCHI INAKOENDA, NYERERE ALIMKEMEA JOHN ASIGOMBEE NCHI ISIJE IKAENDA HUKO SIJUI WAPI, LAKINI LEO NCHI INAENDA WAPI, MNAONA AU MMEFUMABA MACHO AMKENI, SINA CHAMA ILA NAONA MAMBO YANVYOENDA NA KURA YANGU NAJUA WAPI KUIPELEKA JE WEWE?? UNAJUA BAADA YA MIAKA MITANO NCHI HII ITAKUWAJE? UNATASWIRA GANI KICHWANI KWAKO?? NA UNAFANYA MAAMUZI MAZITO GANI KUHAKIKISHA HILO HALITOKEI MIAKA MITANO IJAYO???...UKIWA MZIMA UNITAFUTE BAADA YA HIYO MIAKA MITANO IJAYO BAADA YA KUONA NCHI ULIYOSHINDWA KUIFANYIA MAAMUZI MAGUMU ILIKO!!!

    SHAURI YAKO, VIJIPEASA VAYAKO, ELIMU YAKO TENA VIJIPESA VYA WIZI, UJANJA UJANJA. VITAKUHENYESHA MIAKA MITANO IJAYO...

    michuzi ole wako uniweke kapuni kama kapu la redio tanzania zamani.

    ReplyDelete
  14. hatujamsikia JK akitisha watu, kama Dr. Slaa!

    Slaa ni dikteta...tumeyaona hayo toka kamati ya "wazee wa Chadema"!

    Slaa aliahidi kumchapa mtu mmoja wa Chadema huko sehemu za kusini. Slaa, acha kuwafanya wa-Tanzania watoto wadogo wako wa kuchapwa chapwa!

    Aliahidi kutunga sheria ya kulazimisha watu wasijenge nyumba za nyasi. Kila sheria ina matokeo yake. Wakikataa, atafanyaje? Atawafunga jela!

    ReplyDelete
  15. CCM inawaungansha Watanzania wote, chadema inajaribu kujenga chuki katika nyonyo za Watanzania.

    ReplyDelete
  16. Ni bora tubadilishe jina tu sasa na kuwa WWW.MICHUZI-CCM.BLOGSPOT.COM , Nawasilisha

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...