



Kaka Salama ?
Pole na kulizungusha Durudumu (GURUDUMU), Leo wakati nimechelewa kwenye foleni naelekea kwa ofisi kulizungusha DURUDUMU Nilikutana na hili.
Na ndo raha ya kutembea na hivi vimweku mweku vyetu, Ila itabidi nije unifundishe jinsi ya kutumia Bulakiberi, Yangu inachukua snapu, lakini sijuagi ata kutuma kwa EM EMU ESI, walahi tena.
Ukitoka Unguja basi niambie nije hata ofisini au pale sehemu yetu ya ghahawa japo unikochi kwa sekunde, maana uwa nakutana na ma iventi kedekede, lakini yahe sijui kuitumia, mie nilinunua kwa ajili ya kupokea na kupiga tu, kumbe walahi Hii Bulaki beri yangu ina manjonjo kedekede, wlahi mpaka inachanganya ati.
Hii lori imetumbukia kwenye daraja, yaani sijui Vipi, hata sielewi, Sasa cha ajabu REDIO FM MBAO hazikosekani Sehemu kama hii, nilipohoji majibu yalikuwa kama Ifuatavyo
Wa Kwanza,
“Hapana dreve Alikuwa amechoka akamuachia UTINGO aselebuke, yeye akawa auchapa Siti ya nyuma, Halafau si unajua Bwana usingizi unaambukizwa, UTINGO naye akaanza kuuchapa huku anasuka steringi, loo Kuhamaki Yuko chini ya daraja MATUMBI”
Wa Pili
“ Hapanaaa, Dreve aliona MALUWE LUEW yanavuka barabara , ndo kusema ayakwepe, hamadi, chini ya Daraja Matumbi"
By
Mdau Addo
Afu ndo mnalilia wawajengee barabara za juu kwa juu na madaraja ya uhakika.Vitu vidogo kama hivi mnashindwa kuvitumia kwa uangalifu sasa wakijenga hizo "sky-way" Rd na madaraja si ndo vifo vya kishenzi vitaongezeka kila siku.
ReplyDeletemdau wa kwanza umenena, tutakuwa tunaporomokewa kila siku!cjui tuwekage na ngao kwa juu ili walau iwe inadhurika gari walau sisi tusizikwe bila kutambuliwa. loh!barabara za juu?sasa hili likishuka unafkiri wanaenda wangapi? madereva wajinga na ubovu wa magari vitatuua hata tukijenga barabara alfu angani
ReplyDeletesasa hili black mamba mbona jana halikwenda kibaha jamani maiti 4 zililaliwa na roli masaa kibao hadi zikapondeka?turudi kwenye hii ajali sasa dereva kama ulichoka si mngepaki pembeni mkapumzika jamani usingi na kuendesha gari wapi na wapi jamani.
ReplyDeleteKaka mtoa maoni wa mwanzo big up sana!
ReplyDeleteSkyways hazina maana kwa nchi kama hii kutokana na sheria kutofuatwa na vyombo husika kama nchi jirani tu, yaboreshwe maisha ya mtu wa kima cha chini halafu skyways baadaye 2050 au zaidi. Ulizia madereva wa bongo wa magari ya masafa marefu wanavyotwangwa faini nchi jirani kwa makosa ya kizembe. Hili lori litakuwa limetumbukia darajani usiku wakati magari yakiwa machache mno barabarani, nini tatizo - uzembe? ulevi? ubovu wa gari?
KK
Magamba coast
Hizi leseni za kununua.
ReplyDeleteEti watanzania tunataka barabara za kupita juu kwa juu, mbona itakuwa mauaji ya kila siku!!
ReplyDeleteMatunda ya kutuma SMS-text barabarani!
ReplyDeleteHatuko serious na usalama barabarani hata kidogo.
ReplyDelete1 leseni nyingi ni fake na
zinatolewa na polise hao hao
2 zaidi ya nusu yamagari bara
barbarani ni mabovu kabisa
3 kagua bima za magari, mengi
hayan bima, mbele ya macho yetu
4 piki piki ndio usiseme,watu
wanadiriki kuendesha pikipiki
za namba ya chassis mbele ya
traffic officer bila
kuchukuliwa hatua yoyote
5 SHERIA ZA USALAMA BARABARANI
ZIMEPITWA NA WAKATI NA HAFIFU
MNO
Simlaumu dereva hawana REST AREA sasa gari kubwa namna hii angeli park wapi?
ReplyDelete