Katibu Mkuu wa CECAFA Nicholas Musonye wa kwanza kushoto akipokea Mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni 675 kutoka kwa Mkurungenzi Mkuu wa SBL wa nne kushoto Bw.Ajay Mehta kulia ni Caroline Ndungu Mkurugenzi wa Masoko SBL na katikati ni Meneja Mkuu wa Mawasiliano na Uhusiano SBL Teddy Mapunda na Meneja bidhaa wa SBL Dada Nandi Mwiyombela.

Kampuni ya bia ya serengeti ISBL) kupitiam bia yake ya Tusker imedhamini mashindano ya chalenji kwa jumla ya shilingi miloni 675 za kitanzania kwa ajili ya kuendesha mashindano hayo ikiwa ni pamoja na kugharamia tiketi za ndege kwa timu shiriki na maafisa wa CECAFA pamoja na marefa, malazi, usafiri wa ndani, uratibu, zawadi, ada mbalimbali, usalama, gharama za kutumia uwanja, usajili wa waandishi wa habari na gharama nyinginezo.

Michuano hiyo inatarajiwa kuanza tarehe 27 Novemba mpaka tarehe 11 Desemba mwaka huu ambapo mashindano hayo yanafanyika hapa nchini kwa mwaka huu.

Mashindano ya CECAFA mwaka huu yatashirikisha timu kutoka Kenya, Uganda, Rwanda, Burubdi, Djibouti, Somalia, Ethiopia, Sudan, Tanzania, Zanzibar Eritrea na kwa mara ya kwanza CECAFA imeialika timu ya Ivory Coast kama timu mwalikwa wa mashindano hayo.

SBL ndiyo mdhamini mkuu wa mashindano hayo ya CECAFA 2010 kupitia kinywaji chake cha TUSKER.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Mashindano haya yatafanyika hapa nchini na Itazishirikisha timu za TANZANIA pamoja na ZANZIBAR.
    Siku hizi kuna google translator hizi page zinajiweka wenyewe kwa lugha zakigeni jamani tuangalie!

    ReplyDelete
  2. jamani kwani zanzibar sio Tanzania? duuu hii kali sasa huko tuendako mmm cjui kama tutafika.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...