Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikata utepe kufungua rasmi jengo la Chama Cha Waalimu Tanzania Mkoa wa Ruvuma leo asubuhi.Wapili kushoto ni Rais wa Chama Cha waalimu Tanzania Bwana Gratian mkoba na watatu kushoto ni Waziri wa Elimu Profesa Jumanne Maghembe.
Mwanafunzi wa shule ya msingi Samora mjini Songea mkoani Ruvuma akimkaribisha Rais Jakaya Kikwete kwa saluti maalumu muda mfupi kabla ya Rais Kikwete kufungua rasmi jingo la Chama Cha waalimu mkoa wa Ruvuma leo asubuhi
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwasalimia baadhi ya watoto waliomlaki muda mfupi baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa songea ambapo alikuwa mgeni rasmi katika maadhimnisho ya sherehe ya siku ya mwalimu duniani.
Sehemu tu ya mamia ya waalimu toka mikoa yote nchini waliohudhuria sherehe za siku ya mwalimu duniani wakimsikiliza Rais Dr. Jakaya Mrisho Kikwete alipowahutubia katika uwanja wa michezo wa Majimaji mjini Songea. Rais Dr.Kikwete alikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho hayo kwa mwaliko wa Chama cha Waalimu Tanzania
Mamia ya waalimu waliohudhuria maadhimisho ya siku ya mwalimu duniani wakiingia kwa maandamano katika uwanja wa michezo wa Majimaji mjini Songea ambapo Rais Dr.Jakaya Mrisho kikwete alikuwa mgeni rasmi na kuwahutubia.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. mkandamizajiOctober 05, 2010

    kaka michuzi hongera kwa blog bomba!

    langu ni moja tu muwe waangalifu mnapo-post vyeo vya watu! Mtu huwezi kutambuliwa kama Dr kwa PhD ya kupewa (honorary Phd). U-Dr ni strictly academic qualification, please!...

    Haya ibanie na hii maana unabania nyingi za kwangu!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...