Bosi wa TAKUKURU Dk. Edward Hosea


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
YAH: UCHUNGUZI KUHUSU TUHUMA ZA RADA

Tunapenda kuujulisha umma kuwa uchunguzi na ushahidi uliokusanywa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) pamoja na Shirika la Upelelezi - SFO la Uingereza kuhusu tuhuma za Rushwa katika ununuzi wa Rada, umeshindwa kumhusisha Bw. Andrew Chenge katika tuhuma hizo.


TAKUKURU inawaomba wananchi waendelee kutoa ushirikiano kwa chombo hiki kwa kutoa taarifa za kuwafichua wale wote wanaojihusisha na Rushwa kwani jukumu hili ni la kila mmoja wetu.

Imetolewa na
Doreen J. Kapwani,
Afisa Uhusiano-TAKUKURU
Novemba 08 , 2010
S. L.P. 4865,
Dares Salaam.


Simu: 2150043-6/2150360
Nukushi: (022) 2150047
Baruapepe:dgeneral@pccb.go.tz
Mtandao www.pccb.go.tz

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 16 mpaka sasa

  1. Weldone TAKUKURU!!!! watanzania tumezoea saana kuamini bila ushahidi kama kuna mtu ana DATA awapelekee TAKUKURU now! CHENGE Hongera and Go a head for the speaker's seat

    ReplyDelete
  2. Kama ni kweli akuhusika ktka kesi hii basi hatuna cha kusema.ila waliousika wapewe adhabu kali sana

    ReplyDelete
  3. mkandamizajiNovember 08, 2010

    weweeeeeeeeeeeeeee! chenge for speaker! go CCM!

    ReplyDelete
  4. Ingekuwa vizuri PCCB wangeweka hiyo ripoti ya SFO ya Uingereza nasi wadau tukaisoma kujiridhisha na utendaji wa PCCB(Takukuru).

    ReplyDelete
  5. mmmh,mmeanza sasa!mbona hankusema kabla ya uchaguzi!

    ReplyDelete
  6. SAWA wazee tumesikia!
    Lakini vile vijithumni mmebahatika kujua vimetoka wapi?!
    au na hilo pia mmefeli?
    maana vile ndo chanzo ya vyote.

    tunahitaji maelezo yaliyokamilika and not muhtasari tu.

    ReplyDelete
  7. Kumekucha..who is next? Bongo tambarare .....

    ReplyDelete
  8. hii ndio chama CHUKUA CHAKO MAPEMA never learn from mistake sasa watawafishwa wote

    ReplyDelete
  9. NIMEOTA NDOTO TANZANIA IMEKUWA NA ADABU,UAMINIFU NA HESHIMA,HAKUNA MTOA RUSHWA WALA MPOA RUSHWA,VIONGOZI WANATIMIZA AHADI ZAO BILA YA KUWADANGANYA WANANCHI ILA KABLA YA NDOTO HII KUTIMIA NIMEOTA NDOTO BAHARI YA HINDI SAMAKI WAKIELEA ELEA KILA UPANDE KWA FURAHA WAKILA NYAMA ZA MIILI YA WANADAMU WALIOKUFA KWA KUTOKUWA WAAMINIFU NA NCHI,WATOTO NA NDUGU YA WALE WALIOUAWA WAKILIA KWA UCHUNGU WAKISEMA TUNGEJUA TUSINGE MEGA MKATE AMBAO SIO JASHO LETU WALA JASHO LA BABA ZETU BALI NI JASHO LA MTU AMBAYE HAKUPEWA HAKI!!!KISHA NIKASIKIA SAUTI IKISEMA KWENYE NDOTO HAYA YANAPASWA KUTOKEA KARIBUNI ILI HIYO ADABU,UAMINIFU NA HESHIMA VIJE!!!MWENYE MASIKIO NA ASIKIE

    ReplyDelete
  10. Any suspect will remain INNOCENT until proven guilty in the competant court of law.

    Tatizo letu Tanzania, vyombo vya habari na vyenyewe vimeacha kufanya kazi zake kwa misingi ya maadili badala yake vinafanya kazi kwa ushabiki. Jambo hili linawanyima wananchi/wasomaji habari sahihi na hatimaye kuwajaza wasomaji hao na wananchi mambo ambayo ni ya upotoshaji.
    Kwa mfano, taarifa za kutohusishwa Chenge na tuhuma za rada zipo, lakini hakuna mwandishi ambaye alifanya juhudi za kufuatilia kwa wakati mwafaka na kuwajulisha watanzania kuwa Mh Chenge hakupatikana na dai lolote, badala yake tumeendelea kuachwa kwamba anahusika.

    Tuliona wakati wa uchaguzi mkuu jinsi ya baadhi ya vyombo vya habari vilivyofanya kura za maoni zilizo ratibiwa nje ya utaalam na kumpa hisia mgombea fulani wa urais kuwa ile ndiyo projection sahihi ya matokeo ya uchaguzi. matokeo yake mmempa kiwewe hadi leo anashindwa kuamini matokeo ya kura halisi.

    Vyombo vya habari vinatakiwa vifanye kazi kwa misingi ya uadilifu na si ushabiki.

    ReplyDelete
  11. Htas off Doreen...tunataka uwazi jinsi hiyo...maana mngeendelea kukaa kimya watu wasiomtakia mema wangeanza kuleta hoja za rada na vijisenti ili mradi tu kutaka kumzibia nia yake ya kuwania uspika...binafsi nina imani kubwa naye...naamini anao uwezo..namkumbuka alipokuwa mjumbe wa bodi yetu ya rift valley Seed zama hizo..MUNGU akujaalie kaka Andrew

    ReplyDelete
  12. VIONGOZI WOTE WA TANZANIA KUNA SIKU MTAUWAWA HAZARANI MAPINDUZI YAKITOKEA WASHENZI SANA NYIE WADANGANYE MALIMBUKENI TUMECHOKA NA MWISHO WENU UNAKARIBIA

    ReplyDelete
  13. Doreen, hebu elezea vizuri kuhusiana na hizi tuhuma...haya maswali humu ndani yalijibiwa kweli??
    Ripoti ya SFO hii hapa...

    http://www.scribd.com/doc/11490017/SFO-Report-on-the-Radar-Saga

    ReplyDelete
  14. BAE Systems plc
    05 February 2010
    BAE Systems plc

    The Serious Fraud Office ("SFO") and the US Department of Justice ("DoJ"), have both announced settlements with BAE Systems plc, in a ground breaking global agreement. The DoJ agreement involves BAE's business dealings in a number of countries, whilst the SFO agreement concentrates on the company's operations in Tanzania.

    The SFO has today reached an agreement with BAE Systems that the company will plead guilty in the Crown Court to an offence under section 221 of the Companies Act 1985 of failing to keep reasonably accurate accounting records in relation to its activities in Tanzania. The company will pay £30 million comprising a financial order to be determined by a Crown Court judge with the balance paid as an ex gratia payment for the benefit of the people of Tanzania.

    In conjunction with this agreement the SFO has taken account of the implementation by BAE Systems of substantial ethical and compliance reforms and the company's agreement with the DoJ announced today, and has determined that no further prosecutions will be brought against BAE Systems in relation to the matters that have been under investigation by the SFO.

    SFO Director Richard Alderman said, "I am very pleased with the global outcome achieved collaboratively with the DoJ. This is a first and it brings a pragmatic end to a long-running and wide-ranging investigation. I would like to thank the Ministry of Defence Police for their support and contribution. Furthermore, I'd also like to acknowledge the efforts made by BAE to conclude this matter and I welcome its declared commitment to high ethical standards".

    Zaidi:

    http://www.sfo.gov.uk/search.aspx?search_two=tanzania

    Nawakilisha kaka Mithupu!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...