Dr. JOHN ELTON LUSINGU- Mwenyekiti –TANZ- UK


SIKUKUU YA UHURU/KUMKARIBISHA BALOZI

Zikiwa zimebaki siku mbili tu kabla watanzania kutoka sehemu mbalimbali hawajakutana kwenye ukumbi wa

Stratford Old Town Hall, 29 The Broadway, London E15 4BQ

kusherehekea ile siku muhimu ya uhuru, Jumuiya ya waTanzania TANZ-UK , kama waandalizi wakuu wa shughuli hii tunapenda kutoa utaratibu wa tiketi na maelezo ya ziada kama wengi wenu ambavyo mmekuwa mkiuliza.

TIKETI: TIKETI ZIKO TAYARI NA ZITAUZWA UKUMBINI KUANZIA SAA SITA MCHANA SIKU HIYO YA TAREHE 11-12-2010.

Kwa wale watakaohudhuria Professional Networking Forum mchana hakuna kiingilio ila ticketi za sherehe RASMI za uhuru zitakuwa zinauzwa wakati wa break. Vocha zenye thamani ya paundi tano zitakasambazwa kwa wote watakaohudhuria forum. Kila mwenye vocha hiyo atapata punguzo la paundi tano wakati wa kununua tiketi.

USAFIRI: Ukumbi uko kilomita moja na nusu kutoka Stratford station. Stratford iliyo zone 3 ni kituo kikubwa kikiziunganisha Central Line, Jubilee Line, DLR, Overground, National Express na C2C trains. Car Parking ipo.

Hali ya Hewa: GOOD NEWS! Hali ya ubaridi inategemewa kupungua. Kutakuwa na snow maeneo ya Kaskazini ya Uiengereza ila haitegemewi kusababisha matatizo yoyote. Soma habari kamili hapa (source BBC Weather)

Monday 6 December 2010 to Sunday 12 December 2010

More fog, frost and snow problems

A front will cross northern parts of the British Isles in the first part of the week, producing significant snowfall for Northern Ireland, Scotland ad the north of England.

By midweek, the same front may give further snowfall across the southern half of Britain, but this shouldn't amount to more than a few centimetres.

As winds hover between north and northwesterly, so snow showers may continue to pepper the coasts of northern Britain and Northern Ireland.

The latter part of the week should be less cold as a developing high produces a maritime-based, northwesterly wind. This may feed patchy rain into western parts during Thursady and Friday. Eastern areas should be dry.

Ziada: Kutokana na jinsi ambavyo watu wengi wamekuwa wakiuliza kuhusu siku hii, tunategemea ukumbi utafurika. Hakikisha unapata tiketi yako mapema siku hiyo.

mobile no: 07424530228

email: tanzuk@ymail.com

website: www.watanzaniauk.com

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. Ukumbi uko kilomita moja na nusu kutoka Stratford station? Huu ni upotoshaji mkubwa saana, labda mwandishi alitaka kusema mita 1,500 kutoka station. Ni karibu mno.

    ReplyDelete
  2. Usichanganyikiwe wangu hii ni hesabu ya primary svool 1km = 1,500m

    ReplyDelete
  3. Ama kweli hii ni globu ya jamii, Dr. John Elton Lusingu, nimefutahi sana kukuona kwenye blogu hii, habari za miaka tele. Mimi Mtoto wa Mama Neema wa Ikizu Mission. Makongoro Sec.

    ReplyDelete
  4. sasa hiyo LOGO yao mbona mikono 2 wa wazungu inashake ? au Tz watu wake ni wazungu ? ilitakiwa mkono mmoja uwe mweusi na mwingine mweupe ,ukiwakilisha tz na uk

    ni mtazamo wangu tu..

    mdau UK

    ReplyDelete
  5. WATANZANIA WENZANGU TUUNGANE KATIKA HILI NA TUSHEREHEKEE PAMOJA. NAMSHUKURU MWEYEKITI KWA KUTUPA TAARIFA RASMI YA SHEREHE HII. KWANI KUNA KIKUNDI CHA WAKENYA WAKISHIRIKIANA NA WATANZANIA WAWILI WANAJARIBU KUTUMIA SIKU YETU KATIKA KUFANYA BIASHARA NA KUWADANGANYA WATANZANIA KUWA SHEREHE IKO AMBASSADOR KILABU. JAMANI TUWENI MAKINI NA WATU HAO KWANI PALIPO BALOZI NDIPO SHUGHULI RASMI ITAKAPO FANYIKA. asanteni

    ReplyDelete
  6. Samahani michuzi, mimi kwa kawaida huwa siweki maoni yangu hapa lakini leo naomba unipe nafasi kuweka maoni yangu.

    Dr John elton, website yenu ni aibu kubwa sana, ina clutters nyingi zisizo na maana kabisa, na hazisaidii lolote.

    Nimejaribu kujisajili, na baada ya kujibu masuali yote nimepata ujumbe kuwa hamuwezi kunisajili kwa sasa nijaribu baadae, nimejaribu mara tatu bila mafanikio. Sasa kama huduma hii bado haiko tayari ni kwa nini mumeiweka? kwa nini hamsubiri hadi ikamilike na ndio muweke link yake?

    Mambo ndio hayo hayo kwenye links nyingi kama za photo gallery, ta london, ta manchester na ta reading zote hazina kitu, what the point?

    Pia kuna haja gani kuwepo na link ya money transfer (ambayo pia haifanyi kazi)? kuna haja gani ya kuweka matangazo ya kazi za nyumbani? (pia hamna nafasi za kazi hata moja) kama kuna mtu au kampuni nyumbani inataka kutangaza kazi surely itatumia website zilizopo nyumbani kwa sababu nyingi malipo ikiwa moja wapo.

    Cha kushangaza zaidi hata link ya about us haina kitu, kama hii website haiko tayari kwa nini mumeiweka live? kulikuwa na haja gani ya kuharakisha kuiweka hewani website hii?

    kusema kweli kwa namna ilivyo hivi sasa inaonyesha wazi kuwa hamna plan katika kudesign website hii, designer na developer wenu either ni mwanafunzi asokuwa na experience au ni mtoto mdogo kwani binamu yangu mwenye umri wa miaka 12 anaweza kudesign website nzuri well planed and designed than this.

    Come on Dr John, hivi kweli unataka kutwambia kuwa wewe mwenyewe binafsi umeiona website hii na kuridhika kuwa iwekwe hewani ikiwa na makosa namna hii na kutokamilika?

    Ni aibu sana kwa watanzania kwani website hii inatakiwa kuwatuwakilisha watanzania sote hapa uk.

    I hope katika mkutano jumamosi hii watatokea watanzania wenye taaluma za kudesign na kudevelop website ambao utaweza kuwatumia kui-redesign website hii.

    Ahsante sana
    mr_taymour@hotmail.co.uk

    ReplyDelete
  7. Jamani naomba kuuliza wale wanao deal na mambo ya SISIEM mbona wamekuwa wakimya hizi siku.Jamani mtauwa uSISIEM

    ReplyDelete
  8. Nadhani ndugu hapo juu ana point ila wasiwasi wangu ni kwamba anaweza kuwa mmoja wa wale wale ambao maneno mengi ila hakuna vitendo.
    Jumuiya inahitaji wataalam katika nyanja mbali mbali hivyo ujitokeze na kushiriki kikamilifu sio kutoa lawama tu.
    Pia kama kweli unaona kuna jambo kwa nini usitume email kwa wahusika ili utoe mawazo yako professionally
    Kama nilivyosema hapo juu wasi wasi wangu mdau huyu ni wale wale.

    ReplyDelete
  9. watanzania wenzangu wote wanao taka kusoma ugaibuni London.
    wannaotaka kuwa na uhakika wa kupata UK VISA na 2 years work permit.
    habar njema imefika
    watembelee www.westbound-tz.co.uk

    ingia London ndani ya siku 30

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...