Menaja masoko wa kampuni ya Ngano ya Azania Mohamed Bashrahil wapili kushoto akimkabidhi jezi Mwenyekiti wa timu ya Waandishi Waandishi wa habari za michezo nchini (Taswa FC), Majuto Omary katika hafla fupi iliyofanyika kwenye Mgahawa wa Hadees jijini. Taswa Fc itapambana na timu ya Baraza la Wawakilishi siku ya Sikukuu ya Mapinduzi Januari 12, 2011 kwenye uwanja wa Amaan mjini Unguja. Kampuni hiyo pia ilikabidhi jezi kwa timu ya Baraza la Wawakilishi, Tanzania Stars na timu ya Zanzibar Veterani.wengine ni Mkurugenzi wa Popular Sports and Entertainment Tanzania (PSET), Othman Kazi na wa pili kulia ni Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Kampuni ya Azania, Awadh Fuad.

KAMPUNI ya Ngano Azania imekabidhi jezi seti nne kwa timu ya waandishi wa habari za michezo nchini (Taswa FC), Baraza la Wawakilishi, Tanzania Stars na timu ya Zanzibar Veterani kwa madhumuni ya kutumika katika mechi maalum za kusheherekea sikukuu ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Jezi hizo zilikabidhiwa na Meneja Masoko wa Kampuni ya Ngano ya Azania, Mohamed Bashrahil katika mkutano na waandishi wa habari jana uliofanyika kwenye ukumbi wa Hadees.

Bashrahil alisema kuwa sababu kubwa ya kutoa msaada huo ni kutambua umuhimu wa maendeleo ya michezo nchini na vile vile kama sehemu yao ya kutambua Muungano wa Tanzania na hasa Sikukuu ya Mapinduzi.

Alisema kuwa sikukuu ya Mapinduzi ni kielelezo ya Muungano thabiti wa Tanzania Bara na Visiwani na wao kama kampuni ya Muungano inayofanya kazi zake katika sehemu zote mbili.

“Masoko yetu yapo Tanzania Bara na Visiwani, tunaamini kwa kupitia msaada huu, watanzania watatambua nini tunafanya japo tupo katika biashara muda mrefu sasa, msaa

da huu ni kielelezo tosha cha kutambua Muungano thabiti,” alisema Bashrahil.

Alisema kuwa jezi seti nne zina thamani ya sh. Milion 2.4 na mbali ya hizo jezi, watasaidia vifaa mbali mbali kama kofia, fulana na jezi za kupashia viungo moto au warm up.’

Kwa mujibu wa Bashrahil, wataendelea kusaidia michezo kwani msaada huu ni mwanzo tu wa kielelezo cha ubora wa bidhaa zao na kampuni kwa ujumla.

Mwenyekiti wa Taswa FC, Majuto Omary aliishukuru kampuni hiyo kwa msaada mkubwa waliotoa kwani wanaamini timu zote nne zitapendeza siku ya sikukuu hiyo.

Majuto alisema kuwa “Sikukuu bora ni kuvaa nguo mpya” hivyo wanaamini kuwa msaada huo utaongeza ari za wachezaji na kuibuka na ushindi siku hiyo.

Mkurugenzi wa Popular Sports and Entertainment Tanzania (PSET), Othman Kazi aliishukuru kampuni ya Azania kwa msaada huo na kwani imechangia kufanikisha adhma ya kampuni yake iliyoandaa mechi hizo maalum.

Kazi alisema kuwa ni heshima kubwa kwa kampuni ya Azania na kupunguza ‘presha’ ya bajeti kubwa ya PSET iliyoandaa shughuli hiyo.

“Naziomba kampuni nyingine ziunge mkono Azania na kusapoti PSET ili kufanikisha shughuli hiyo nzito na muhimu kwa Watanzania,” alisema Kazi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. safi sana azania , ndo inavyotakiwa hivi kusaidia mambo mbalimbali katika jamii, hongera bashrahil


    mdau
    S.A.J

    ReplyDelete
  2. Asanteni kampuni ya Azania kwa kujali michezo nchini!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...