Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na bango
la 'Uhuru Kamili' Tisa Desemba, 1961
Meja Alexander Gwebe Nyirenda akifikisha mwenge wa Uhuru kwenye kilele cha Mlima Kilimanjaro usiku wa kuamkia siku ya Uhuru ili umulike nje ya mipaka yote, uleteeeee tumaini. Meja Alexander Gwebe Nyirenda na mwenye
wa Uhuru alioupandisha Kilimanjaro.
Afande huyu ni mmoja wa mashujaa wa
Uhuru wasioimbwa (Unsung Heroes)

Mwalimu Julius Nyerere na Meja Nyirenda
wakati wa mnuso wa siku ya Uhuru.

Soma mahojiano ya Meja Nyirenda BOFYA HAPA

Jikumbushe historia kamili ya Tanganyika BOFYA HAPA

Siku aliyotutoka Meja Nyirenda BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Hivi Tanganyika tulipata UHURU au haki ya kujitawala wenyenyewe??!! Maana hatukuwa koloni bali tulikuwa tukiandaliwa tu kujitawala.
    Hivyo pale tulipojitutumua na kuonyesha basi tunaweza basi Mwingereza akasema, " Mtoto akililia wembe, mpe" Tukapewa sasa angalia tunavyojikatakata wenyewe.
    Hivyo mimi nahisi kusema tulipata uhuru si sahihi maana sisi baada ya vita kuu ya kwanza tuliwekwa chini ya Uangalizi kwa amri ya Umoja wa Mataifa wa wakati ule (league of nations).
    Itakuwa vizuri kama hili likasawazishwa.

    Kwa maneno mengine sisi tulikuwa tukiongozwa au kusimamiwa na Waingereza hatukuwa tunatawaliwa kama Wakenya.
    Naomba kutoa hoja hiyo.
    Mzawa

    ReplyDelete
  2. KifimbochezaDecember 09, 2010

    Waandishi wa habari mmeamua kuharibu Kiswahili kweli kweli. Nyie ndo mnategemewa kuwa watetezi wa Kiswahili lakini si hivyo. Tusiharibu Kiswahili chetu kwa direct translations. "Unsung heroes" = Mashujaa wasiotajwa mara kwa mara. Si mashujaa wasioimbwa!

    ReplyDelete
  3. Wewe Michuzi, tafuta ukweli wa kauli hii:

    "Meja Alexander Gwebe Nyirenda akifikisha mwenge wa Uhuru kwenye kilele cha Mlima Kilimanjaro usiku wa kuamkia siku ya Uhuru..."

    Ukweli: Usiku wa kumakia siku ya Uhuru, hali ya hewa haapo killeni Kilimanjaro ilikuwa mbaya sana kutokana na tufani kubwa la theluji na upepo. H

    Hivyo, Nyirenda hakufikia kileleni. Ilibidi auache huo mwenge chini kidogo. Baadaye, yaani siku za baaaye, ndipo ulipopandishwa kileleni!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...