Kaka Michuz hapa nilipo nipo katikati ya watu kuna mgomo mkubwa sana wawanachuo wote wa Chuo Kikuu cha Dodoma University (UDOM) wakidai kupewa Field work katika vitivo mbalimbali hapa chuo.

Wanafunzi wanadai wamejaribu kuongea na uongozi wa chuo lakini hawaoni maendeleo yoyote hivyo kimeitishwa kikao cha dharula kwa wanachuo wote, na kudai kufanya mgomo kuanzia kesho

bado nasubiri nikipata picha ntazituma!
MDAU UDOM

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Mgomo uliopo ni wa wanafunzi wanaosoma kwenye College of Humanities and Social Sciences(Chuo cha Sayansi ya Jamii) na sio UDOM yote. chuo cha Elimu(College of Education), College of Hearth Sciences, na College of Informatics na Schools nyingine zote ndani ya UDOM kupo shwari na wanafunzi wanaendelea na masomo kama kawaida.

    Mdau kutoka UDOM

    ReplyDelete
  2. Hawa Vijana wanadhani migomo ni ujanja! Wajifunze kuwa sehemu ya kutoa ufumbuzi wa matatizo yanayo ikabili jamii yetu na sio migomo ya hovyo hovyo.

    Migomo ndiyo inayodhoofisha elimu ya juu Tanzania. Kuna baadha ya anasiasa wana tumia fursa hiyo kuhamasisha migomo kwa wanafunzi vyuoni, hiyo ni siasa mbovu ambayo hatuitaki nchini.

    Vijana wetu wanahitaji kueleweshwa madhara ya migomo vyuoni. Kwa upande wa uongozi wa vyuo na waasa kusikiliza na kujali matatizo ya wanafunzi wetu wa vyuo. Wakati mwingine viongo husika wamekuwa waki dharau na kuonyesha kupuzia concerns za wanafunzi na hivyo kuwaongezea hasira na baadaye kufanya migomo.

    Ifike mahali huo utamaduni wa migomo vyuoni utoke kabisa kwa manufaa ya taifa letu.

    Mdau wa Elimu, Tanzania.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...