Afisa wa Ufadhili wa kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Ibrahimu Kaude akimkabizi simu mshindi wa Vodacom Miss XXL After scholl Bash,Amisa Hussein wa Sekondari ya Tandika ya jijini Dar lililowashilikisha wanafunzi wa pamoja wa shule za sekondari,kipindi hiki cha likizo katika Hoteli ya Kunduch Beach.katikati ni mtangazaji wa Clouds Tv Zamaradi Mketema.

Afisa wa Ufadhili wa kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Ibrahimu Kaude akimkabizi simu mshindi wa Vodacom Mr XXL After school Bash,Karama Haji wa sekondari ya Tusiime katika shindano lililowashilikisha wanafunziwa pamoja wa shule za sekondari,kipindi hiki cha likizo katika Hoteli ya Kunduch Beach.kulia ni mtangazaji wa Clouds TV .Zamaladi Mketema.
Mwanamuziki mahiri Joe Makini akiwapagawisha wanafunzi waliofika katika Tamasha la Vodacom XXL After School Bash lililofanyika katika Hoteli ya Kunduchi Beach lililokuwa na lengo lakuwakutanisha wanafunzi wote katika kipindi hiki cha Likizo.
Msanii chipukizi kutoka kundi la Tip Top Connections Dogo Janja akiwarusha wanafunzi wa shule mbalimbali katika tamasha la Vodacom XXL After school Bash lililofanyika katika Hoteli ya Kunduchi Beach.likiwa limeandaliwa na Vodacom kwa kushirikiana na CLOUDS.
Mwanamuziki wa kizazi kipya Mwasiti akikonga nyoyo wanafunzi wa shulembalimbali waliohudhulia katika Tamasha la Vodacom XXL After School Bash lililofanyika katika hotel ya Kunduch Beach

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. Jamani wenzetu katika tamasha hili mlitumia kigezo gani kupata washindi? Nauliza hivi maana msijekuitwa washamba kama tulivyoitwa WASHAMBA na Master J kwenye mashindano ya BSS kwa ajili ya kumshabikia mzungu Joseph Pyne.

    Niliumia sana kitendo cha Master J kukashifu watu au naweza kusema kutukana watu (pengine watanzania) kwa ajili ya kumpigia kura mzungu Joseph Pyne; na si kumpigia kura tu, hata kule kumshabikia alipoimba jukwaani.

    Mimi nauliza kwa Master J, ni kigezo kipi cha ushamba alichokiona? Ni nani alimchagua mzungu Joseph Pyne kuingia kwenye BSS? KAMA NI USHAMBA, BASI MASTER J NA MAJAJI WENGINE NDIWO WASHAMBA MAANA WAO NDIWO WALIMCHAGUA PYNE KATIKA MSULULU WA WAIMBAJI WENGI WALIOJITOKEZA KUWANIA NAFASI.

    Nilikuwa nafuatilia sana mchakato wa kuteua washindani, hata mikoani mlikokwenda, nilikuwa nafatilia, maana mlikuwa mnaonyesha kwenye runinga
    Joseph Pyne alianza kwenye foleni kama wengine walivyoanza. Nakumbuka Joseph Pyne siku moja aliingia na gita katika usaili (interview) ya BSS. Miongoni mwenu mlimsisitizia sana NA KUMSHAURI Joseph aimbe kiswahili. Nadhani ushauri ule mlimpa kwa kuwa mliona ana kipaji hata mkampa nafasi. Nauliza, walikuwa watu wangapi kutoka Dar, lakini Pyne mliona anakipaji hata mkamchagua. Kwa kipaji hicho hicho mlichokiona Watanzania na watu wengine walikiona na ndiyo maana walikuwa wanampigia kura na pia kumshabikia. Haikuwa ni kwa sababu ya uzungu wake, bali ni kwa vitu alivyokuwa anafanya. Sasa iweje kutuita WASHAMBA?

    Master J, pengine njia mliyochagua ya kumpata mshindi huenda mmekosea. Kama kutuma SMS tu ndiyo kura zenyewe za kupa mshindi, basi hakuna haja ya kuwatukana watu na kuwaita washamba.

    MKURUGENZI WA BENCHMARKER, MADAM RITA, ULIUONA UDHAIFU HUU? HATA KAMA MASTER J ALIKUWA NA MTU WAKE ALIYETAKA ASHINDE, HAIKUWA NA SABABU YA KUKASHIFU WATU NA KUWAITA WASHAMBA. TENA LIVE, MOJA KWA MOJA, HADHARANI.
    WENYE BUSARA ZETU TULISIKITIKA SANA. KITENDO KILE NAOMBA KILAANIWE. HUKU NI KUPUNGUKIWA NA BUSARA.

    Hitimisho. KAMA MASTER J AMEKOMAA KIMAADILI, ANAPASWA KUWAOMBA RADHI WATU (MASHABIKI) KWA KUWAKASHIFU KUWAITA WASHAMBA.

    Ni mimi Busara si Mvi

    ReplyDelete
  2. Naunga mkono hoja hii. Nakuomba Ankel Michuzi, ikiwezekana peleka ujumbe huu kwa Master J, na Madam Rita Paulsen wajirekebishe. Vinginevyo, wasituhamasishe mashabiki kutuma msg kuwapigia kura wale tuwapendao. Wapigieni wenyewe sasa ninyi mlio werevu. Au lengo lenu ni kutaka tuwachangie kupitia sms zetu tu halafu mnaishia kutukashfu?

    Hongera mdoa duku duku, kumbe uliguswa kama mimi.

    ReplyDelete
  3. hamkudhalilishwa chochote ila mmeambiwa ukweli. wabongo au waafrica kwa ujumla acheni kushobokea wazungu..huku kwao hufiki hata second round hata kama una sauti ya kumtoa nyoka pangoni..kama mnabisha waulizeni watu wa UK walivyoona jinsi watu weusi walivyobaguliwa kwenye mchakato mzima wa X-Factor!!! nimefurahi mshindi ni mzawa at least mtu mmoja au tuseme familia moja ishajitoa katika umaskini...Big up Madam Rita na Master J.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...