Habari toka kwa ripota wetu huko Dodoma zinasema Waziri Mkuu Mh. Mizengo Kayanda Pinda aka 'Mtoto wa Mkulima' amewasili Chuo Kikuu cha Dodoma mchana huu na hivi tunavyoongea anapita kila mahali ukagua majengo na miundombinu ya chuo hicho asmbacho kikikamilika kitakuwa na uwezo wa kubeba wanafunzi 40,000.

Mh. Pinda, huku akishangiliwa na wanafunzi na waalimu ambao wanaonesha kufarijika kwa ujio wake ambao huenda ukaondoa kwikwi kibao zinazowakabili, amepitia mabweni, madarasa na hata vyoo na kujionea hali halisi. Inatarajiwa ataongea na wanafunzi na wafanyakazi mwishoni.

stay tuned!

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. DAAH afadhali mzee wetu uje kutuokoa manake huku si shwari

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...