Balozi Ali Mchumo

Wiki hii shirika la Umoja wa mataifa la chakula na kilimo FAO limesema bei ya chakula dunia imefurutu ada mwezi wa Januari mwaka huu

Gharama za chakula kama ngano, mahindi, sukari na mafuta ya kupikia imekuwa ya juu kuliko wakati mwingine wowote. FAO inasema bei zimekuwa zikipanda kwa miezi saba iliyopita na inaonekana itaendelea katika miezi ijayo.

Ngano, mahindi, sukari na bidhaa za maziwa imepanda kwa asilimia kati ya 3 na 6 kwa mwezi Januari mwaka huu wa 2011. Hali hii imesababisha kufanyika kongamano la kimataifa mjini Geneva Uswis kuhusu kupanda kwa bei ya chakula, athari zake na njia za kukabiliana na tatizo hilo. Kongamano hilo limeandaliwa na shirika la Umoja wa mataifa la masuala ya bidhaa na biashara UNCTAD na kuhusisha FAO, shirika la mpango wa chakula duniani WFP na wadau wengine.

Miongoni mwa waliohudhuria ni balozi Ali Mchumo ambaye ni mkurugenzi mtendaji wa mfuko wa pamoja wa masuala ya bidhaa wa UNCTAD. Amezungumza nwa mwandishi wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa mjini Geneva Patrick Maigua na kuanza kumueleza nini sababu kubwa ya kupanda kwa bei ya mazao duniani.

Kwa kina bonyeza links hizi kusikiliza

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...