Waandamanaji wa Misri wakimba nyimbo
kumtaka rais Mubarak kuondoka mara moja.

Rais Barack Obama ametoa wito wa kuwepo na kipindi cha mpito kitakachopelekea kundwa serikali itakayo sikiliza matakwa ya wananchi. Viongozi wa Ulaya kwa upande wao wametoa wito wa kuwepo na uchaguzi wa huru na haki katika taifa hilo la Kiarabu lenye wakazi wengi.

White House ilieleza Jumapili kwamba rais Obama alizungumza na viongozi wa Uingereza, Uturuki, Israel na Saudi Arabia mnamo siku mbili zilizopita. Alirudia nia ya serikali yake ya kuwepo hali ya kustahmiliana wakati inaunga mkono haki za kidemokrasia kwa wananchi wa Misiri ikiwa pamoja na haki ya kukusanyika pamoja kwa amani na haki ya kujieleza.

Mhadhiri wa chuo kikuu cha Florida Charels Bwenge anasema Marekani inajikuta katika hali nzito, kwa upande haiwezi kumtupa rafiki yake wa muda mrefu katika utaratibu wa amani na wakati huo huo inaunga mkono mabadiliko ya kidemokrasia kwa wamisri.

Habari kamili tembelea VOA

BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Hosni is as old as Mugababe. Kwasababu tu ni kibaraka wa Marekani na Uingereza hawajambatiza kama DICTATOR! Maslahi kwanza demokrasia baadae.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...