Zoezi la utoaji wa Kili Tanzania Music Awards lilipomalizika hapo juzi pale Diamond Jubilee Hall jijini Dar-es-salaam,jina moja lilibakia katika vinywa na bongo za mashabiki wa muziki na wote waliofuatilia tuzo hizo.Jina hilo sio lingine bali la Abbas Hamisi au maarufu kama kwa jina la kisanii la 20%.
Kijana huyo mzaliwa wa mkoa wa Pwani ambaye unaweza kusema bado ni msanii asiyejulikana sana hususani nje ya mipaka ya Tanzania,aliibuka “Mfalme” kwa kutwaa jumla ya tuzo 5 miongoni mwa vipengele 7 alivyokuwa ameteuliwa katika kuwania tuzo hizo.
Kwa ujumla 20% aliibuka mshindi kama Male Artist of The Year(Msanii Bora wa Kiume), Best Male Singer(Mwimbaji Bora wa Kiume), Best Song Writer of The Year(Mwandishi Bora wa Nyimbo wa Mwaka) na huku kibao chake cha Tamaa Mbaya kikiibuka mshindi katika kipengele cha Best Song of The Year(Wimbo Bora wa Mwaka) na Ya Nini Malumbano kikiibuka mshindi katika Best Afro Pop Song(Wimbo Bora wa Afro Pop).
Kwa bahati mbaya, 20% hakuwepo ukumbini kupokea tuzo zake na badala yake producer wake John Shariza “Man Water” kutoka Combinations Sounds ndiye alikuwa na kazi ya ziada ya kuzibeba tuzo 5 za 20%.
kuona mahojiano yaliyofanywa baina ya 20 % na BongoCelebrity
BOFYA HAPA
Kijana huyo mzaliwa wa mkoa wa Pwani ambaye unaweza kusema bado ni msanii asiyejulikana sana hususani nje ya mipaka ya Tanzania,aliibuka “Mfalme” kwa kutwaa jumla ya tuzo 5 miongoni mwa vipengele 7 alivyokuwa ameteuliwa katika kuwania tuzo hizo.
Kwa ujumla 20% aliibuka mshindi kama Male Artist of The Year(Msanii Bora wa Kiume), Best Male Singer(Mwimbaji Bora wa Kiume), Best Song Writer of The Year(Mwandishi Bora wa Nyimbo wa Mwaka) na huku kibao chake cha Tamaa Mbaya kikiibuka mshindi katika kipengele cha Best Song of The Year(Wimbo Bora wa Mwaka) na Ya Nini Malumbano kikiibuka mshindi katika Best Afro Pop Song(Wimbo Bora wa Afro Pop).
Kwa bahati mbaya, 20% hakuwepo ukumbini kupokea tuzo zake na badala yake producer wake John Shariza “Man Water” kutoka Combinations Sounds ndiye alikuwa na kazi ya ziada ya kuzibeba tuzo 5 za 20%.
kuona mahojiano yaliyofanywa baina ya 20 % na BongoCelebrity
BOFYA HAPA
Asalaam alaykhum 20%. Napenda sana nyimbo zako kuanzia ile ya kwanza kabisa iliyokutoa nyimbo inaitwa BINTI KIMANZI kisha ukatoa nyimbo inatwa MONEY MONEY ohhhh safi sana kaka real nakubali sana kazi yako ya kutyunga nyimbo pamoja na kuimba. Mola akupe nguvu na afya njema tunednelee kuburudika.
ReplyDeleteChef Issa