Mkurugenzi Mkuu wa Radio Karagwe FM Bw. Emmanuel Muga (kulia) akiwa studio na Mkuu wa Wilaya ya Karagwe Col. Fabian Massaw, ambaye hualikwa studio mara kwa mara kujibu maswali moja kwa moja kutoka kwa wasikilizaji wa redio hiyo. Radio za Jamii zimezidi kuenea nchini kote na Radio Karagwe FM ni moja ya redio zinazoongoza mkoani Kagera.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. Vizuri sana Karagwe, huu ni mfano mzuri wa kuigwa kwani local news siku zote huwa ni muhimu....

    Sisi tunaotokea Mwanjelwa bado tunasikiliza radio za Dar.. ninajua siku zijazo tutaweza kuwa na uwezo wa kuweka kitu kama hichi..

    Brother Michu ahsante sana kwa kuweka habari kama hizi..

    ReplyDelete
  2. Naona huko nyuma kuna chupa ya Serengeti Beer? Vipi watangazaji hupata kilaji kwanza kisha wakaingia hewani?

    ReplyDelete
  3. Mkuu wa wilya KARAGWE = MASSAWE???

    ReplyDelete
  4. Hee! Mwanjelwa hakuna Radio?mbona huku Kyela tuna Radio yetu muda mrefu tu sasa tumeshaachana na ushamba wa kusikiliza mambo ya Dar...kwanza wala hatukujui.

    ReplyDelete
  5. Anon namba mbili yaelekea umepoteza uwezo wa kuona .ina bidi ukapige One Cup kwa Babu, hiyo chupa inaonekana kabisa ni ya maji, we unasema Serengeti. yaelekea mdau sana wa kilaji hata maji waita pombe.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...