
Vitu vilivyotolewa na benk hiyo ni pamoja na unga wa Sembe, Mchele, Unga wa
Ngano, Mafuta ya Kula ,Sukari, Chumvi,Maharagwe, Sabuni na Nguo.
Mkuu wa Mpango Mkakati na Mahusiano ya Benki Jaffer Mlachano alikabidhi vitu hivyo kwa niaba ya benki kwa Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Mecki Sadiki ambapo alitoa rai kwa taasisi nyingine kama wao pamoja na wadau mbalimbali kuendelea kujitokeza kusaidia waathirika husika.
Alisema msaada huo ni katika kuthamini utu wa watanzani wenzao waliopatwa na mkasa huo ambao kwa namna moja au nyingine ni nguvu kazi ya taifa hivyo
wanapaswa kufarijiwa kwa kuwapa msaada.
“Tumesikitika na kuguswa kwa namna ya kipekee na tukio lililowapata wenzetu nasi kama miongoni mwa wadau tunatoa msaada wetu wa vyakula na vitu vingine na wale waliojeruhiwa tunawaombea wapone haraka,”alisema
Kwa upande wakeKaimu Mkuu wa Mkoa aliishukuru benki hiyo na kuiomba kuongeza tena msaada mwingine kama uwezo utawaruhusu kwani mahitaji bado ni mengi.
“Tunawashukuru kwa jinsi mlivyoguswa na kuamua kujitolea kwa kiasi
mlichoweza,lakini bado tunatoa rai kwenu na kwa wadau wengine kujitolea zaidi endapo uwezo unawaruhusu kufanya hivyo kwani mahitaji bado ni mengi”, alisema
mkuu huyo.
Alisema pamoja na watanznaia kuonyesha moyo wa kujitolkea kwa kadri uwezo
ulivyowaruhusu lakini bado Serikali inaamini waathirika husika wataendelea
kuishi kwa kutegemea misaada hiyo kwa kipindi kirefu kijacho kabla ya kurudi
katika hali zao za kawaida kimaisha hivyo wadau bado wanaombwa kujitokeza
kusaidia.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...