Na Francis Godwin wa Globu ya Jamii,Iringa
CHAMA cha mapinduzi (CCM) mkoa wa Iringa kimetoa muda wa siku saba kwa mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Nduli, Ayubu Mwenda na diwani wa kata ya Nduli, Idd Chonanga kumaliza tofauti zao zilizoibuka baada ya kura za maoni ndani ya CCM mwaka 2010.
Hatua hiyo imekuja baada ya wananchi wa kijiji hicho kulalamika mbele ya katibu wa CCM mkoa wa Iringa Mary Tesha kuwa kijiji hicho kwa sasa kimesimama kufanya shughuli za kimaendeleo baada ya viongozi hao kupingana wenyewe na pale mmoja anapoitisha mkutano ya hadhara mwingine huzuia wananchi kuwa hakuna kwenda katika mkutano .
Wakitoa malalamiko yao mbele ya katibu huyo wakati wa ziara yake ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa leo ,wananchi hao walisema kuwa toka kumalizike kwa uchaguzi mkuu mwaka jana kijiji hicho hakuna shughuli yeyote ya maendeleo ambayo imekuwa ikifanyika na chanzo ni diwani na mwenyekiti wa serikali ya kijiji hicho ambao wamekuwa wakipingana.
Walisema kuwa hivi sasa wananchi wamekuwa wakiichukia CCM kutokana na viongozi hao kutofautiana na kuwa bado CCM imeshindwa kuchukua hatua zozote za kumaliza tatizo hilo .
Hivyo walitaka CCM kuwavua uongozi diwani na mwenyekiti wa serikali ya kijiji hicho kutokana na kuendekeza makundi ya kisiasa na mivutano isiyomalizika.
Pia wananchi hao walisema kuwa katika kijiji hicho kumekuwepo na ufisadi mkubwa wa fedha za makusanyo ya mnala wa simu ,ardhi pamoja na kuwepo kwa kero kubwa ya maji na huduma za afya pasipo kushughulikiwa na viongozi hao ambao wamekuwa wakiendekeza malumbano zaidi.
Kwa upande wake katibu wa CCM wilaya ya Iringa Charlesy Charlesy alisema kuwa CCM wilaya imepata kushughulikia kero hizo japo inashangazwa na hatua ya wananchi kuendelea kuibuka malalamiko zaidi.
Alisema kuwa chama ngazi ya wilaya kimefika mara kadhaa katika kijiji hicho kutatua malumbano hayo ya diwani na mwenyekiti wake .
Huku naibu meya wa Manispaa ya Iringa Gervas Ndaki akiwataka viongozi hao kutenganisha siasa na utendaji katika kuwashughulikia wananchi hao .
“Mambo ya siasa yaende kisiasa na serikali yaende kiserikali wasichanganye mambo katika utekelezaji wa maendeleo ya kijiji cha Nduli…tengenezeni ratiba ya mikutano ya serikali “
Katibu wa CCM mkoa wa Iringa ,Tesha alisema kuwa anatoa siku saba kwa viongozi hao kumaliza tofauti zao na kuvunja makundi ya uchaguzi na kama siku hizo zitamalizika bila kuvunjwa kwa makundi hayo kati ya diwani na mwenyekiti wake ambaye alikuwa mgombea katika kura za maoni nafasi ya udiwani ndani ya CCM basi chama kitachukua hatua dhidi yao.
CHAMA cha mapinduzi (CCM) mkoa wa Iringa kimetoa muda wa siku saba kwa mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Nduli, Ayubu Mwenda na diwani wa kata ya Nduli, Idd Chonanga kumaliza tofauti zao zilizoibuka baada ya kura za maoni ndani ya CCM mwaka 2010.
Hatua hiyo imekuja baada ya wananchi wa kijiji hicho kulalamika mbele ya katibu wa CCM mkoa wa Iringa Mary Tesha kuwa kijiji hicho kwa sasa kimesimama kufanya shughuli za kimaendeleo baada ya viongozi hao kupingana wenyewe na pale mmoja anapoitisha mkutano ya hadhara mwingine huzuia wananchi kuwa hakuna kwenda katika mkutano .
Wakitoa malalamiko yao mbele ya katibu huyo wakati wa ziara yake ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa leo ,wananchi hao walisema kuwa toka kumalizike kwa uchaguzi mkuu mwaka jana kijiji hicho hakuna shughuli yeyote ya maendeleo ambayo imekuwa ikifanyika na chanzo ni diwani na mwenyekiti wa serikali ya kijiji hicho ambao wamekuwa wakipingana.
Walisema kuwa hivi sasa wananchi wamekuwa wakiichukia CCM kutokana na viongozi hao kutofautiana na kuwa bado CCM imeshindwa kuchukua hatua zozote za kumaliza tatizo hilo .
Hivyo walitaka CCM kuwavua uongozi diwani na mwenyekiti wa serikali ya kijiji hicho kutokana na kuendekeza makundi ya kisiasa na mivutano isiyomalizika.
Pia wananchi hao walisema kuwa katika kijiji hicho kumekuwepo na ufisadi mkubwa wa fedha za makusanyo ya mnala wa simu ,ardhi pamoja na kuwepo kwa kero kubwa ya maji na huduma za afya pasipo kushughulikiwa na viongozi hao ambao wamekuwa wakiendekeza malumbano zaidi.
Kwa upande wake katibu wa CCM wilaya ya Iringa Charlesy Charlesy alisema kuwa CCM wilaya imepata kushughulikia kero hizo japo inashangazwa na hatua ya wananchi kuendelea kuibuka malalamiko zaidi.
Alisema kuwa chama ngazi ya wilaya kimefika mara kadhaa katika kijiji hicho kutatua malumbano hayo ya diwani na mwenyekiti wake .
Huku naibu meya wa Manispaa ya Iringa Gervas Ndaki akiwataka viongozi hao kutenganisha siasa na utendaji katika kuwashughulikia wananchi hao .
“Mambo ya siasa yaende kisiasa na serikali yaende kiserikali wasichanganye mambo katika utekelezaji wa maendeleo ya kijiji cha Nduli…tengenezeni ratiba ya mikutano ya serikali “
Katibu wa CCM mkoa wa Iringa ,Tesha alisema kuwa anatoa siku saba kwa viongozi hao kumaliza tofauti zao na kuvunja makundi ya uchaguzi na kama siku hizo zitamalizika bila kuvunjwa kwa makundi hayo kati ya diwani na mwenyekiti wake ambaye alikuwa mgombea katika kura za maoni nafasi ya udiwani ndani ya CCM basi chama kitachukua hatua dhidi yao.
Mmegundua kwamba chama chenye demokrasia komavu kuliko vyote nchini ndicho chama pekee ambacho baada ya uchaguzi watu wanatakiwa "kuvunja makundi"?
ReplyDelete