Waziri wa Maji,Prof. Mark Mwandosya akimkaribisha Mbeya mgeni wake, Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi ya Aliance For Green Revolusio in Africa (AGRA), Dr. KOFFI ANNAN pindi alipowasili katika uwanja wa Ndege wa Mbeya.kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya,Mh. John Mwakipesile.Dr Annan akiwa mkoani mbeya atatembelea Taasisi ya ARI UYOLE na skimu ya umwagiliaji iganjo mbeya vijijini atatembelea Duka la pembejeo lusungo shamba la mahindi la mfano Mbozi atatembelea shamba la mfano la soya mbimba duka la pembejeo iyula na kuona bidhaa mbalimbali zinazozalishwa kutokana na soya
Dr. Koffi Annan akiangalia ngoma ya asili ya kinyakyusa ifahamikayo kama lighoma pindi alipowasili katika uwanja wa Ndege wa Mbeya.Dr Annan ambaye kwa sasa ni mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa AGRA (Aliance For Green Revolusio in Africa) inayojihusisha na masuala ya uboreshaji wa kilimo na utafiti katika nchi za Afrika
MWAMBIE AHAKIKISHE ANAPATA KIKOMBE KABLA HAJAONDOKA!!!
ReplyDeleteHapo Kofi kapata mwenyeji wa ukweli! Yaani Mwandosya na Koffi kwa appearnce na usomi wanaendana kabisa!
ReplyDeleteHAKO KA AIRPORT KANATIA AIBU SERIKALI DOOOO
ReplyDeleteaaah sasa mbona mbunge wa mbeya mr sugu hayupo wakati wageni wamefika jimboni kwake au kila kitu ni usisiemu
ReplyDeletemisupu usibane
Anonymous # 2,
ReplyDeleteWaafrica mnakazania wasomi wasomi mbona mnashindwa kuiendeleza Africa na wasomi wenu? Wezenu akina Mark Zuckeberg(Facebook), Bill Gates(Microsfot), Michael Dell(Dell Copmuter) wamebadilisha dunia bila hata kuwa na degree moja.Mafundi baiskeli Wright Borthers wamebadilisha dunia kwa kutengeneza ndege bila hata kuwa na huo usomi mnaoupa kipaumbele. What about a farm boy Henry Ford?
Amka kaka!
Michuzi tafadhali huwa huweki maoni yangu mimi nikiandika ndo kwanza mada inafungwa sio vizuri ankal.Mimi napongeza sana jitihada za Mh.Waziri namwona ni mtu anayefanya mambo kwa uwezo mkubwa sana kt kila wizara anayogusa.The prof is very humble.kupata mawazo kutoka kwa wazoefu na wenye maadili kama hawa kina Koffi ni jambo jema na la maendeleo kwa Taifa.hongera kaza buti mhesh.waziri.
ReplyDeleteMimi nimeona mambo mawili tu la kwanza wahusika wa Mkoa au uwanja wa ndege hayo maandishi juu ya bati si sahihi na ukichukulia watu toka nje wanapitia hapo neno sahihi ni AIRPORT na si AIR PORT. Jambo la pili ni ktk picha ya pili hilo bango la nguo neno la kwanza nalo si sahihi SUPPOPT usahihi ni SUPPORT, hivi hapakuwa na ukaguzi wa mambo kabla mgeni hajafika? Kumbukeni hizi picha zinakwenda mbali na ni aibu kwa Taifa
ReplyDeleteMdau