Ndugu Wanachama,

SIKU YA MWISHO YA KUCHUKUA FOMU ZA UONGOZI NI

JUMAPILI, MAY 8, 2011.

TAREHE YA UCHAGUZI NI JUMAPILI MAY 22, 2011. KATIKA UKUMBI WA 2200 TANGLEWILDE HOUSTON, TX. 77063, KUANZIA SAA 8 MCHANA MPAKA SAA 4 USIKU.

Kwa kukumbushia tu nafasi zitakazogombaniwa ni hizi zifuatazo;

Mwenyekiti wa Tawi na,
Wajumbe kumi wa Halmashauri kuu ya Tawi.

Kwa wale wanachama wanaoishi mbali na mji wa Houston,TX. Kamati ya uchaguzi inafanya utaratibu wa kuwawezesha kupiga kura mapema (early voting), mara tu majina ya wagombea wote yatakapojulikana.

Kwa maelezo zaidi wasiliana na kamati ya uchaguzi katika ccmmarekani@gmail.com au ingia http://ccmmarekani.blogspot.com

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI,

Abdallah Nyangasa

Kaimu Katibu Mkuu,

CCM-Marekani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. Kaka

    Naomba kupata kujua viongozi wa tawi la Chicago

    ReplyDelete
  2. Mbona CHADEMA NA CUF hawana matawi Ughaibuni?

    ReplyDelete
  3. Hizi habari za kuanzisha matawi ya vyama vya siasa ugaibuni ni upuuzi mtupu na zinaweza hata kuleta kutokuelewana wenyewe kwa wenyewe,tumekuja kutafuta maisha huku ili tuweze kujikwamua kutoka katika umasikini uliopo nchini mwetu,nawashangaa hawa wenye muda wa kushughulika na vyama vya namna hii,ikiangalia kwa makini vyama hivi hivi ndivyo vinavyolalamikiwa kwa ufisadi na kusababisha maisha kuwa mabaya nyumbani,na ndiyo maana tukakimbilia huku ugaibbuni,hatupendelei kuishi huku ila ni maisha mabovu ndiyo yanatukimbizia huku,Halafu unasikia watu wanaleta mambo ya chama ugaibuni,huu ni upuuzi mtupu,tumieni nguvu zenu kutafuta maisha kama ni vyama ni nyumbani ambako watu wana muda wa kupoteza.
    Mtoa maoni Ugaibuni.

    ReplyDelete
  4. Marekani kubwa, unaposema tawi la CCM Marekani unamaana gani na unajaribu kumdanganya nani? Just say tawi la CCM Houston or TX but not Marekani.

    ReplyDelete
  5. Tafakari - CCM Marekani haina gamba la kujivua???????

    ReplyDelete
  6. Hatutaki upuuzi wa vyama ugaibuni,maana hasa hasa tutajikuta tunatetea mafisadi tu,hakuna mjinga anayetaka mambo ya vyama vya kisiasa huku.
    Ugaibuni.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...