Mwakalebela akitoka katika chumba cha mahakama na kulakiwa na mama yake mzazi (kulia) pamoja na wananchi wa Manispaa ya Iringa baada ya kushinda kesi yake kwa mara ya pili
Maofisa wa Takukuru mkoa wa Iringa wakiwa hawaamini kilichotokea leo mahakamani baada ya mahakama kwa mara ya pili kuitupilia mbali kesi ya Mwakalebela
Mwakalebela na mkewe Celina wakiwa kizimbani kabla ya kuachiwa huru na mahakama leo


Kwa mara nyingine aliyekuwa mshindi wa kura za maoni ndani ya CCM na aliyekuwa katibu mkuu wa TFF Frederick Mwakalebela na mkewe Celina wameibwaga vibaya mahakamani taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) mkoa wa Iringa katika shitaka lao la kudaiwa kutoa rushwa wakati wa mchakato ndani ya CCM wa kutafuta ridhaa ya wana CCM kugombea nafasi hiyo.

Mbele ya hakimu wa mahakama ya Iringa Mh. Mary Senapee ,Mwakalebela na mkewe waliachiwa huru leo asubuhi baada ya kuonekana hawana hatia na hawana kesi ya kujibu katika shitaka hilo lililofunguliwa kwa mara ya pili ya Takukuru mkoa wa Iringa.
Habari Kamili toka kwa Francis Godwin itafuata punde

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 26, 2011

    Mwakalebela hakuwa anashindana na TAKUKURU! Hivyo kusema kwamba kaishinda si kweli. TAKUKURU imeshindwa kuthibitisha madai yake dhidi ya Mwakalebela. Zilizokuwepo ni TUHUMA TU! If this was a null hypothesis we'd say IT FAILED TO ACCEPT that Mwakalebela is guilty of...........
    Kilichotokea ni kwamba haki imetendeka.

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 26, 2011

    Jamani nisaidieni ni Lini hawa Jamaa wa TAKUKURU tangu wakiwa TAKURU wameshinda kesi?

    Tatizo ni nini?

    Hawana wataalam wa sheria?
    Hawana ujuzi?
    Wanafanya kazi kwa hisia badala ya utaalamu?
    wanafanya kazi kwa msukumo wa kuambia kamata huyu?

    Nadhani kuna haja ya kufutwa TAKUKURU

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 27, 2011

    jamani naomba niwatetyee hao maofisa wa takukuru ni wanasheria tena nimesoma nao tumaini... poleni sana my collegemates.. pole sana kaka unanikumbusha mbali.... sio mbaya u have failled to prove beyond reasonable doubt this time.. usikate tamaa..... pongezi kwa mwakalebela

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...