
Afisa wa kikosi cha usalama barabarani mkoani Kagera PC Joseph akitoa mafunzo ya udereva kwa madereva toka maeneo mbalimbali yaliyoko wilayani Muleba, kikosi hicho kinatoa mafunzo hayo kwa kushirikiana na chuo cha udereva cha Lake zone kilichokopo mkoani Kagera ambacho kimejizazititi kwa kutoa ushirikiano na jeshi la polisi katika juhudi za kupambana na ajali za barabarani

Mkurugenzi mkuu wa chuo cha Lake Zone Bw. Wiston Kabantega akiwaelezea madereva namna ya kujiepusha na ajali wakati wa mafunzo ya udereva yanayotolewa na jeshi la polisi mkoani Kagera kwa kushirikiana na chuo hicho yanayoendelea wilayani Muleba katika ukumbi wa Calfornia.

Mrajisi msaidizi mkoani Kagera Juma Mokili akitoa ufafanuzi wa baadhi ya maswali yaliyokuwa yanaulizwa na wajumbe wa mkutano mkuu wa chama cha ushirika mkoani Kagera.

Inamuonyesha mwenyekiti wa chama cha ushirika mkoani kagera (KCU) john Binushu akitoa taarifa kwa wajumbe wa chama hicho wakati wa mkutano mkuu ulioandaliwa na chama hicho ambao ulifanyika jana katika hoteli ya yassila uliokuwa mahsusi kwa ajili ya kutoa ufafanuzi wa mizania. Picha na Audax Mutiganzi wa Globu ya Jamii, Kagera
Hii ni habari nzuri, keep it up. Kazaneni kwa waendesha pikipiki pia. Maana huku Dar siku barabara za watembea kwa miguu na pikipiki hazijulikani wote tunakwepana humohumo
ReplyDelete