Salaam Kaka,
Nipo safarini huku Newala na hili ni eneo linaloitwa kitangari,lipo wilaya ya Newala,ni kilometa 30 kutoka eneo linaloitwa Mtama barabara kuu ya lami itokayo lindi kwenda masasi.Leo niliweza mwenyewe kuongea na bibi huyo hapo pichani anaeitwa Luwungi,nikamuhoji kuwa ilikuwakuwaje,akanambia kuwa alipata habari hizo ndotoni na kwamba moyoni mwake alisikia sauti ikimwamba awape watu dawa hiyo.

Pia bibi huyo anasema alipata kuanza shughuli hii tangu tarehe 6 mwezi April mwaka huu.hakuna tofauti sana katika ugawaji dawa kama kule semunge,loliondo.

Nimeona msururu mrefu wa watu wakisubiri dawa hiyo ambayo inasemekana kutibu magonjwa ya kifua kikuu,ukimwi na mengineyo sugu kama arobaini kwa ujumla wake.

ni hayo tu kaka kwa leo
mdau Hussein safarini Newala.
Dozi ya Vikombe ikiwa tayari kwa kupewa waagonjwa.Mbele ya Kikombe hata ukali wa jua hauonekani.
Watu Nyomii katika eneo hilo.
Foleni ya kusubiria dozi ikiwa imekomaa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 02, 2011

    Eh! Mbona naona kama bibi ana maandazi pembeni(Picha ya kwanza)? Au hicho kikombe unasukumia na andazi ili dawa ifanye kazi ipasavyo?

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 02, 2011

    Ikiwa watu wengi namna hii, maana yake hata dawa inatibu. "Clinical trial" safi kabisa hiyo wasomi wa Muhimbili na UDOM na Kariuki. Taarifa za wanasayansi wetu walioifanyia utafiti dawa ya Babu ni kuwa inatibu hayo magonjwa sugu. Sasa kilichobaki mgariga upandwe nchi nzima.

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 02, 2011

    Patamu hapo yule wa sumange atakwambia yeye ndio anayemilki

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 03, 2011

    Namshukuru mungu tumepata kikombe cha kwetu, maana ilikuwa ni ngumu kusafiri kutoka Tandahimba hadi semunge Loliondo.

    Mdau Belgium

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 03, 2011

    anagalieni afya zenu kwanza kila mtu atasema kaoteshwa basi tufunge hoapital hakuna haja ya kua na hosptali tusuburi wanao oteshwa watibu jamani ndoto zimepanda zinashinda upako

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 03, 2011

    Michuzi mbona hujatuambia bei ya kikombe,Watanzania tuko juu kwa tiba,sasa hakuna tena kwenda Hospitali.Mungu endelee kutuotesha tufunge Hospitali zote...maskini madaktari wajifunze kulima sasa!

    ReplyDelete
  7. AnonymousMay 03, 2011

    Watz mnatia huruma, hivi mnajua thamani ya miili yenu? mbona mnaabuse miili mlipewa na Mungu,? Mi natamani mngejiuliza kabla ya kunywa, halafu bado mnasali au mmesha acha? tutajua vizuri ikifika mwisho wa yote haya maana kila chenye mwanzo kina mwisho na kama wametumwa na Mungu aliyeumba vyote inabidi walokole mjue kwani biblia inasema Mungu hakutuficha lolote, itasikitisha itakapogundulika ametumia mkojo, kinyesi (bora kiwe cha wanyama kuliko cha binadamu)au damu ya wale watoto waliookotwa jalalani ndo mtalia na wakati huo mmeshabugia.Halafu huyu ni mganga.Poleni ila akili zenu zifunguke kwa jina la Yesu.

    ReplyDelete
  8. AnonymousMay 04, 2011

    we anony wa kwanza kula tano manake unajua kuzichambua picha.Ni kweli dawa shurti ishushiwe na andazi vinginevyo haifanyi kazi. hapo ni bizness x2. unanunua kikombe na andazi pia..hehehehe bongo tambarareeee.

    ReplyDelete
  9. AnonymousMay 04, 2011

    Ukiwa umechuka darasa la abnormal pysch watu wengi watakuwa diagnose na Schizophrenia. haluccination na delusional criteria zimewakilishwa toka babu aje na kikombe. Ila darasa linasema tanzania na nchi zingine kuna better outcome za wagonjwa kupona kutokana na support ya jamii. Ikimaanisha ukiwa na pych problem tanzania upelekwi hospital ila unatukuzwa kwamba unafanya miujiza. Inanishangaza muda mwingine lakini ndiyo nchi yangu. mwenyezi mungu tusaidie.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...