-Mchezaji wa timu ya Mkoa wa Morogoro , Moro Stars, Dickson Mbeikya ( kulia) akijaribu kufunga kwa kichwa huku Mlinda mlango wa timu ya soka ya Mkoa wa Manyara, Ally Mohamed ( jezi 18) akijiandaa kuokoa mpira huo katika moja ya heka heka zilizotokea langoni mwake , katika mchezo huo wa mashindano ya Kili Taifa CUP , Kituo cha Morogoro uliofanyika jana uwanja wa Jamhuri wa mji Kasoro Bahari. Moro Stars ilishinda bao 1-0.


Mlinda mlango wa timu ya soka ya Mkoa wa Manyara, Ally Mohamed , akiuweka mpira katika himaya ya mikono yake kufuatia shuti kali ililichongwa na mmoja wa washambuliaji wa timu ya Mkoa wa Morogoro, Moro Stars ( hayupo pichani) huku mabeki wa timu yake akihakikisha usalama wake , waksati wa mashindano ya Kili Taifa CUP , Kituo cha Morogoro uliofanyika jana kwenye uwanja wa Jamhuri wa Mjini hapa, Moro Stars ilishinda bao 1-0

Mlinda mlango wa timu ya soka ya Mkoa wa Manyara, Ally Mohamed ( jezi zambarau) akijiandaa kuokoa mpira wakati ilitotokea heka heka langoni mwake katika mchezo dhidi ya Mkoa wa Morogoro, Moro Stars , katika mashindano ya Kili Taifa CUP , Kituo cha Morogoro uliofanyika jana kwenye uwanja wa Jamhuri wa Mjini hapa, Moro Stars ilishinda bao 1-0. Picha na John Nditi wa Globu ya Jamii, Morogoro


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 09, 2011

    Mbona viwanja vyeupe nyie TFF?i.e Hakuna watazamaji wa kutosha...Enzile zile Mwanza Heroes Vs Mzizima United au Rwelu Eagles Vs Mapinduzi Stars...weeeee.Haya Mashindano yaendelee kufanyika Mkoa hadi mkoa kama zamani..Pliiz TFF

    Bwana John Nditi Safi sana kwa picha...CC wengine tuko mbali na Moro.



    David Villa

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...