Hii ni blogu yenye mtazamo wangu na sayansi ya fizikia ya kiatomiki..(kama nitakuwa nimepatia) nina maana ya quantum physics. nataka kuamsha changamoto kwa wenye vichwa vya sayansi walioko katika vyuo vikuu vya Afrika kwa ujumla kwasababu waafrika tumekuwa watumizi wakubwa wa teknolojia na hivyo kutufanya sie kuwa ni soko kubwa kwa makampuni ya nje kuanzia mambo ya vifaa vya mawasiliano na hata vifaa vya matumizi ya nyumbani, mashambani, mahospitalini na kila mahala.
Tunachokosa ni ufahamu wa ndani wa teknolojia hizo. sizungumzii jinsi ya kuripea simu ama friji lako likiharibika bali misingi hasa ya teknolojia hizo. lengo langu ni kuwasha moto wa fikra kwa wasomi wetu walioko Afrika na kwengineko duniani tuweze kujiunga na kumiliki japo sehemu ya ukuaji wa teknolojia hizi. ahsante. Mdau Mwanafunzi.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...