meneja uhusiano mwandamizi wa benki ya Posta,Noves Moses (kushoto) akimkabidhi mkuu wa shule ya sekondari ya Bakoba, Methew Mabruk meza na viti vilivyotolewa na benki wakati wa hafla fupi iliyofanyika katika shule hiyo.
meneja uhusiano mwandamizi wa benki ya Posta tawi la Bukoba, Noves Moses akisikiliza kwa makini wimbo wa shule uliokuwa ukiimbwa na wanafunzi wa shule ya sekondari ya kata ya Bakoba, Bi Moses alikuwa shuleni hapo mwishoni mwa wiki kukabidhi msaada wa meza 50 na viti 50 vilivyotolewa na benki hiyo kwa shule hiyo vyenye thamani ya shilingi milioni 4.5.
kaimu mkurugenzi mtendaji wa manispaa ya Bukoba, Tina Sanga kushoto akiwa amekalia viti na meza vilivyotolewa kama msaada na benki ya posta, anayefuata ni Bi Moses,Mkuu wa shule ya Bukoba, Methew Mbaruk na wa mwisho kulia ni meneja wa benki ya posta tawi la Bukoba Maduhu Makoye.
meneja uhusiano mwandamizi wa Benki ya Posta, Noves Moses akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi wa shule ya sekondari ya kata ya Bukoba, katika picha hiyo aliyevaa suti ni meneja wa Benki ya posta tawi la Bukoba, Maduhu Makoye.Picha na Audax Mutiganzi - Globu ya Jamii,Bukoba

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 16, 2011

    Safi sana Posta.Mimi nimesoma hapo 1986-1989 O-level.Shule iko hapo upande wa Pili wa Posta..Miaka ile kulikuwa hakuna kuvuja mitihani kama sasa.Ukifaulu umefaulu kweli na kihalali.tulikuwa tunashindana kufaulu kati ya Bukoba 'Seko',Kahororo,Ihungo,Nyakato na Rugambwa.Kipindi kile shule za serikali zilikuwa 'zinatesa' si mchezo
    na zilikuwa zinaheshimika sijui kumetokea nini hapa katikati.

    D.Villa

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 16, 2011

    Yaani hakuna sababu ya wanafunzi kukaa chini kwa kukosa madawati. Million 4 madawati 50 na Viti 50? Gari moja inanunuliwa million 70. Kwanini tusijinyime wadogo zetu, watoto wetu, wajukuu zetu wakakaa kwenye madawati Kama sisi tulivyokua tukisoma? Hatuoni aibu? Kweli ntu unakwenda kutembelea shule na gari ya mamillioni na kuwaangalia wanafunzi machoni wakati wamekaa chini!!!! Ni nini serikali inalo la kujitetea kweli?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...