kwa mara ingine tena natanguliza shukuranio zangu za dhati kabisa kwanza kabisa kwako wewe Anko Michuzi na pili kwa wadau wote wa Blogu ya jamii, kwa maoni na ushauri walionipatia kipindi ambacho nilikuwa na uhitaji mkubwa wa mawazo, nasema asanteni sana na mwenyezi Mungu awabariki nyote. 

Lengo langu la leo ni kuwafahamisha kilichojiri baada ya kuomba ushauri wenu. kama wadau wengi walivyonishauri twende Hospitali na kweli kabisa nilifanya hivyo. ila kabla ya yote nilimueleza Ukweli wa hali halisi kwamba nyumbani kwa mfalme suleiman kuna pafyum ambayo hainivutii, basi yeye alijisikia vibaya sana na alilia sana baada ya kusikia maneno hayo, akasema kama kungekuwa na infection yoyote angejua hilo mapema yeye mwenyewe, kwa hiyo yeye mwenyewe furaha ikamtoka kabisa na alilia siku nzima, yeye mwenyewe baada ya kumuambia ukweli akasema inabidi twende Hospitali hata kabla mimi sijapendekeza. basi tukaenda Hospitali akafanyiwa vipimo vyote na majibu ni kwamba hana tatizo lolote na wala hana aina yoyote ya infection. ila DR. aliandika dawa inabidi atumie kwa siku 5. hope mambo yatakwenda vizuri.

kwa mara ingine tena asanteni sana na ninawatakia kila la heri wadau wote wa Blog ya jamii.            
 asanteni sana.

Mdau wa Pwani


NB: Kwa wailokosa mjadala wa mdau huyu 
ama kwa wanaotaka kujikumbusha
BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 30, 2011

    Shukrani na wewe.

    Kuna wengine huwa wana kikwapa cha asili huwezi kukitoa kwa namna yeyote.

    Ndo maana inabidi umchague mweza akiwa hajajipodoa. Akiwa katika worst beaty case.

    Vidokezo vichache ni jasho na ushuzi/ujambo.

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 30, 2011

    mbona sielewi nini kinaongelewa hapa? can u be more specific kwa wasomaji wapya.

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 30, 2011

    na wewe kwa manjonjo!

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 31, 2011

    asante mdau uliyerudi kutoa shukrani baada ya kupata ushauri kutoka hapa umefanya vizuri kushukuru kwani sio woote wanawezakutoa shukrani baada ya kufanikiwa sasa swali langu umesema ulipomweleza ukweli alilia sana hujaweza kumtia moyo kwa kumwambi asifikiri kwakuwa kumweleza ukweli siokwamba unamchukia na wala humwachi bali unampenda ndio maana ukamweleza ukweli maana ungekuwa umpendi ungemwacha kimyakimya hapo angejisikia vizuri enewe siwezikujua ulimfariji vipi lakini umefanya vizuri kumweleza ukweli

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...