Mgeni Rasmi katika uzinduzi wa Filamu ya CHUMO,Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii,Dr. Haji Mponda akitoa hotuba ya uzinduzi wa Filamu hiyo inayoelezea athari za ugonjwa wa Malaria,Uzinduzi huo umefanyika usiku huu katika hoteli ya Movenpick jijini Dar.

Mtengenezaji Kiongozi wa Filamu hiyo,Jordan Riber akizungumza na vyombo vya habari kabla ya uzinduzi wa filamu hiyo katika hoteli ya Movenpick usiku huu.

Mkuu wa Mradi wa COMMIT,Rob Ainslic akizungumza katika uzinduzi huo usiku huu.

Meneja wa Mipango wa Mradi wa COMMIT,Waziri Nyoni akiwafafanulia jambo waandishi wa habari (hawapo pichani)kabla ya uzinduzi wa Filamu ya CHUMO inayoelezea athari za ugonjwa wa Malaria nchini,Katika hoteli ya Movenpick jijini Dar usiku huu.

Stelingi wa Fimumu hiyo,Jokate Mwegelo akizungumza na waandishi wa habari namna alivyoweza kufikisha ujumbe kwa jamii juu ya ugonjwa Malaria.

Mkuu wa Masoko na Ushirikiano wa Benki ya Stanbic,Abdallah Singano akiongea na Waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusiana na ushirika wao katika Mpango wa kudhibiti malaria kwenye ujauzito wakati wa uzinduzi wa filamu mpya inayoelezea athari za ugonjwa huo katika jamii.

kwa picha zaidi 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...