Jumuia ya wanafunzi waliowai kusoma na ambao wanasoma katika shule ya Secondari ya Makongo, wanatarajiwa kufanya Bonanza la aina yake katika viwanja vya Leders Club Kinondoni Jijini Dar es Salaam..

Dhumuni la Bonanza hilo ni kuhamasisha vijana kwa wazee kuwa michezo ni ajira.,Makongo ni moja ya shule ambayo imetoa wanamichezo wengi ambao wamefanya mengi katika sekta ya michezo mbali mbali hapa nchini..

Ratiba kamili ya bonanza hilo ambalo,lifanyika siku ya Jumamosi katika viwanja vya Leders club watu wote wapenda michezo wataalikwa kuja kushiriki katika tamasha hilo,ambapo kingilio kitakuwa shilingi 2000 tu kwa kila mtu.

RATIBA NI KAMA IFUATAVYO

08:00 - 09:00 Asubuhi -Wanafunzi waliosoma na walioko Makongo watajumuika kwa pamoja kufanya Usafi katika eneo lote la shule ya Makongo.

09:00 - 10:00 Dua au Misa kwa ajili ya kuwaombea Walimu na Wanafunzi wote waliosoma Makongo Ambao Wametutangulia mbele za haki.

10:00 - 11:00 Watu wote kutoka katika Shule ya Makongo kuelekea katika Viwanja vya Leders Club Kujumuika kwa pamoja na wadau na wapenzi wa michezo hapa Nchini.

11:00 - 14 : 00 Michezo mbali mbali kuanza,kwa wanafunzi wote, waliosoma na wanaoendelea kusoma Katika shule ya Makongo pamoja na wadau wa michezo kujumuika kwa pamoja.

14:00 - 14 :30 Lisala kwa wanafunzi kwenda Waalimu na Uongozi wa Shule na Lisala kwa wanafunzi wa Zamani kwenda walimu na wanafunzi wa sasa.

16:00 - 18:00 Mechi kati ya wanafunzi wa Makongo na Timu ya Yanga

18:00 - 00:00 Burudani Kutoka kwa Tmk Wanaume,Chege Na Temba,Mapacha wa Tatu,Dogo Janja na Tip Top Connection,Na wengine wengi Kutoka Makongo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 16, 2011

    Hii nembo inaonesha waliosoma makongo ni wazungu...strange idea!

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 16, 2011

    Halafu siyo waliosoma bali aliyesoma kwani FSM imefupisha maneno Former "Student" of Makongo na siyo Former "Students" of Makongo.Inakuwaje jumuiya ya mtu mmoja!Yaweza kuwa mzungu mmoja aliyesoma Makongo.Kazi tunayo!!!.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 16, 2011

    Kwa mwendo huu wa kutojithamini hatutoki!

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 16, 2011

    badilisheni hiyo nembo haifai strange idea kweli kweli

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...