Warembo 15 wanaowania taji la miss DAR INTER COLLEGE kartika shindano litakalofanyika terehe 17 mwezi huuu katika club mpya ya SANSIRO wanaanza kambi ya mzoezi tarehe 6 katika ukumbi wa BRAKE POINT jijini DSM.
Mratibu wa shindano hilo VICTORIA KIMARO amesema kuwa maandalizi yanaendelea mabpo warembo hao wataaanza kujifua nchini ya miss TANZANIA NAMBA 2 wa mwaka 2009 BEATRICE LUKINDO ambaye ni mzoefu katika masuala ya urembo.
VICTORIA amesema kuwa mwaka huu, shinndano hilo litakuwa la iana yake kutokana na warembo waliojitokeza kushiriki kuwa katika ubora wa hali ya juu.
Aidha VICTORIA amewaomba wadhamini zaidi kujitokeza kudhamini shindano hilo ambapo mrembo ROSE JOHN ndiye anashikilia taji hilo. Amewataja wadhamini waliojitokeza ni pamoja na VODACOM,REDDS, NDEGE INSURANCE,MLIMANI MEDIA,CLOUDS TV,PARIS PUB na TRAVEL PARTNER,
Wasanii watakaotoa burudani watatangazwa hivi karibuni
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...