Msanii Francia (kulia) akiwa na Meneja wake Shelamina(kushoto), pamoja na Mtarajiwa Bi Lilian Saidi
Muandalizi mkuu na Mlezi wa Bi harusi mtarajiwa Bi Anande Daniel
![]() |
| Ma MC wa sherehe ya Jikoni Bi Susan Mzee na Makrina Kalinga |
![]() |
| Wageni ktk Sherehe ya jikon |
Bi harusi mtarajiwa na Mpambe wake, wakimeremeta
Dada Maureen na Mariam nao walikuwepo ktk kumfunda mwali huyo
Mtarajiwa na mpambe wake wakisikiliza kwa makini mafundisho kutoka kwa wanawake wengine
Wanawake wa mji wa Reading, UK jana walikusanyika pamoja ktk Kumpa mawili matatu Mtarajiwa Lilian Saidi, anaetegemewa kuolewa hivi karibuni na Bwana Paul Mhando.
Kama kawaida yao wanawake hawa wenye ushirikiano mkubwa sana, walichanga pesa na kufanya sherehe hii ya jikoni, ili kuongea na binti huyu mrembo kuhusu maswala ya ndoa.
Ama kweli wanawake hawa wana mafindisho mazuri, kama hauamini basi hudhuria siku moja kwenye sherehe hizi za jikoni. Na kwakweli tunaona matokeo, kwani ndoa nyingi huko Reading ni moto wa kuotea mbali. Tuige mfano huo.
-Imetolewa na Mdau Mlondoner









kaazi kweli kweli.....
ReplyDeleteJe hao maharusi ni wabeba boksi au watoto wa wabeba boksi?
ReplyDeleteBi harusi mtarajiwa ni mrembo kweli! tunategemea atafuata maadili ya ndoa, mji wa kusoma ni mji wa wana ndoa waliodumisha ndoa zao!big up!!
ReplyDelete