Wachezaji wa timu ya Ulinzi ya Kenya ( jezi nyekudu) wakijipanga kuondosha hatari langoni mwao na kuwadhibiti washambuliaji wa timu ya Soka ya St: George ya Ethiopia ( jezi za njano) katika mchezo wa mashinsano ya kombe la kagame uliofanyika Juni 28, mwaka huu kwenye uwanja wa Jamhuri wa Mjini hapa, timu hizo zilitoka sare ya kufungana bao 1-1.
Beki wa timu ya soka ya Ulinzi ya Kenya ( jezi namba 2 kulia) , Geoffrey Kokoyo akichuana na shambauliaji wa timu ya St George ya Ethiopia ( jezi njano),Atthony Bongole , katika mchezo wa mashindano ya kombe la Kagame , kituo cha Morogoro
Kikosi cha timu ya Soka ya St George ya Ethiopia katia mashindano ya kombe la Kagame kituo cha Morogoro kabla ya mechi ya leo |
Kikosi cha timu ya Soka ya Ulinzi ya Kenya ,inayoshiriki mashindano ya kombe la Kagame , kituo cha Morogoro kabla ya kuvaana na wapinzani wao timu ya St George ya Ethiopia |
Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Said Mwambungu, akisalimiana na mchezaji wa timu ya soka ya Ulinzi ya Kenya , Geoffrey Kokoyo ,kabla ya kuanza mchezo kati yao na timu ya soka ya St: George ya nchini Ethiopia , katika mashindano ya Kombe la Kagame, kituo cha Morogoro , hata hivyo timu hizo zilitoka sare ya kufungana bao 1-1. Picha zote na John Nditi wa Globu ya Jamii, Morogoro
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...