Kiongozi wa kundi la Rugowoile kutoka mkoani Kagera akichekelea kitita cha Tsh. 1,000,000/= baada ya kukabidhiwa na mgeni rasmi wa mashindano ya Ngoma ya Balimi Extra Lager Kanda ya ziwa, Kaimu mkurugenzi wa jiji la Mwanza Bw. Patrick Karangwa. Nafasi ya pili ilishikwa na Utandawazi toka Mwanza na kujipatia kitita cha Tsh. 750,000/= na cha tatu ni Mwenge Sanaa Group toka Tabora na kujipatia kitita cha Tshs. 500,000/=.

Fainali za Mashindano ya Ngoma ya Balimi Extra Lager, zimefanyika Jumamosi tarehe 9/7/2011 katika uwanja wa CCM Kirumba,jijini Mwanza na kufanikiwa kupata kundi la Rugowoile kutoka mkoani Kagera kutawazwa rasmi washindi wa mashindano hayo na kujinyakulia kitita cha Tsh. 1,000,000/=

Katika mashindano hayo yaliyoshirikisha jumla ya vikundi kumi kutoka mikoa ya Mwanza, Kagera, Shinyanga, Mara na Tabora, mshindi wa pili ni kundi la Utandawazi kutoka mkoani Mwanza ambao wameondoka na donge nono la Ths. 750,000/= Mshindi wa Tatu ni kundi la Mwenge Sanaa Group kutoka mkoani Tabora ambao wameondoka na kitita cha Tahs. 500,000/=, Mshindi wa Nne ni kundi la Rugu kutoka mkoani Kagera ambao wamejinyakulia donge nono la Tsh. 400,000/= Mshindi wa Tano hadi wa Kumi wamejinyakulia kitita cha Tsh. 300,000/= kila kundi.
Kundi la Egumba Sanaa Group toka Mara likionyesha umahiri wake.
Kundi la Utandawazi toka Ukerewe wakionyesha umaarufu wao kumiliki jukwaa ambapo kundi hili lilishika nafasi ya pili katika fainali hizo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...