Mwanafunzi wa Kidato nne wa  Shule ya Sekondari Mzumbe ,Josephat Mafung’a ( wapili kushoto) akitoa maelezo ya  vifaa vinavyounda na kufanya kazi katika Kompyuta ,mbele ya Mgeni rasmi , Kaimu Ofisa Elimu wa Mkoa wa Morogoro, MaryRose Lyimo , ( watatu kulia), wakati wa siku ya Kiingereza , Julai 23, mwaka huu, Shule 10 za Sekondari za Morogoro zilishiriki  kwenye shindano hilo lililofanyika kwenye ukumbi wa Sekondari Mzumbe.
Mwanafunzi wa  Shule ya Sekondari ya Kilakala ya vipaji maalumu , akijenga hoja za msingi katika kutetea umuhimu wa taaluma yake ya Uandishi wa Habari mbele ya wanafunzi wenzake  wakati wa siku ya Kiingereza , julai 23, mwaka huu ,Shule  10 za Sekondari za  Mkoa wa Morogoro ,zilishiriki shindano hilo katika  ukumbi wa Shule ya Sekondari ya Mzumbe.
Umati wa wanafunzi wa  shule 10 za Sekondari zilizopo   Mkoa wa Morogoro pamoja na Walimu wao na wageni wengine wakiwa ndani ya ukumbi wa shule ya Sekondari Mzumbe, wakati wa siku ya Kiingereza , Julai 23, mwaka huu, wanafunzi wa shule hizo walishindanishwa   mada mbalimbali zilizohusiana na  masomo
Walimu wa kigeni wanafundisha masomo mbalimbali katika Shule ya Sekondari za Serikali , Mkoani Morogoro wakijumuika na walimu wenzao na wanafunzi wa shule 10  za Morogoro , wakati wa siku ya Kiingereza iliyofanyika  Julai 23, mwaka huu, mada mbalimbali zilishindaniwa  na wanafunzi hao katika   ukumbi wa Shule ya Sekondari  Mzumbe.
Mwanafunzi wa Kidato cha sita mchepuo wa HGL wa Shule ya Sekondari Morogoro , Da' Gwantwa Atilio ,akinogesha muziki mbele ya wanafunzi wenzake na waalimu  siku ya Kiingereza Julai 23, mwaka huu ambayo hushindanisha   mada za masomo mbalimbali, Shule  10 za Sekondari za  Mkoa wa Morogoro ,zilishiriki  shindano hilo kwenye  ukumbi wa Shule ya Sekondari ya Mzumbe, Wilayani Mvomero, Mkoa wa Morogoro. Picha na habari na John  Nditi wa Globu ya Jamii, Morogoro

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...