Waziri wa Habari, Vijana ,Utamaduni na Michezo Dkt Emmanuel Nchimbi akipata maelezo mjini Dodoma juu ya wajibu wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) katika kuwaelimisha wataalamu wa kada hiyo wakati alipotembelea banda la Wizara ya fedha kwenye maonyesho ya wakulima ya nanenane mjini Dodoma.
Waziri wa Habari, Vijana , Utamaduni na Michezo Dkt Emmanuel Nchimbi (katikati) akiwa na Kikundi cha Sanaa za maonyesho Tanzania (KISAMATA) cha jijini Dar es salaam wakati kikundi hicho kikielimisha wananchi wa Dodoma waliotembelea banda la Wizara ya Fedha kwenye maonyesho ya wakulima ya nanenane mara baada ya Waziri huyo kutembelea banda la HAZINA mjini Dodoma.
Waziri wa Habari, Vijana ,Utamaduni na Michezo Dkt Emmanuel Nchimbi akisisitiza umuhimu wa wananchi kujiwekea akiba kwa ajili ya siku ya baadaye wakati alipotembelea Mfuko wa Pensheni(PPF) kwenye banda Wizara ya fedha kwenye maonyesho ya wakulima ya nanenane mjini Dodoma.Kulia ni Afisa Habari wa PPF Edwin Kyungu.





Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...