Ankal,

Hivyo serikali imeagiza ni AMRI kwa polisi kuvaa vizuia risasi – Bullet -Proof vests kwa askari wote wanapokuwa wapo kikazi zaidi, hata kama wapo ofisini wakiandika taarifa mbalimbali. Gazeti la Beeld linaeleza kuwa makamanda wa ngazi zote watashughulikiwa endapo itapatikana kuwa askari walio chini yao hawafuati maagizo hayo.
Hii inakumbusha jinsi ambavyo hali ya uhalifu bado ipo juu hapa SAUZI. Si ajabu hapa kukuta askari wengi wana ‘chamoto ‘ wakati wowote wakitembea. Mapambano ya askari na majambazi mitaani hasa Joberg na Pretoria si mambo ya kushangaza sana hapa.
Pichani ni mfano wa bullet proof vest wanazotakiwa kuvaa askari muda wote.
Labda ndio maana bongo inasemekana ni nchi ya amani sana…eti eehh, mambo haya hayapo !
Mdau, John
Sauzi.
Inafika hatua binadamu anakua haoni tafauti ya kuishi na kufa. Binadamu kama huyo anaweza kufanya jambo lolote. Ndio maisha ya watu wengi wa ughaibuni na raha zote walizonazo. Mtu kuuwa hauni taabu!!
ReplyDelete