MAREHEMU OMARY SAIDI ULEMBO
Leo ni mwaka mmoja tangu ututoke ghafla katika dunia hii. Ndugu yetu Omary Saidi Ulembo, ulituaga ukiwa mzima wakati unaelekea Nairobi Kenya kwa shughuli za kikazi, lakini umauti ulikukuta huko huko na kurejeshwa nyumbani ukiwa marehemu.
Sisi tulikupenda lakini Mola alikupenda zaidi. Mapenzi ya Allah Yatimizwe.
Unakumbukwa zaidi na Mama yako Bi. Husna Omary, Mke wako Sheila Omary, watoto wako, Harith na Shamim, Kaka yako Hidan Omary Ricco, dada zako, Fatuma, Mtumwa, Ziada, Mwanaasha, Lemna, Thureiya, wadogo zako Ngabwe, Rama, Saidi, Shafy, Sadiki, Salum na Juma. Wajomba zako Shanni na Mbwana,
Mama zako akina Mama Mtumwa, Mama Yusuph, Mama Shamte, Mama Ponda, Mama Jongo
bila ya kusahau ndugu, jamaa na marafiki wa karibu, Ali Kirro, Pambwe, Khalfani, Abdalla na wengineo.
Tunamuomba Mwenyezi Mungu ailaze roho yako mahali pema peponi.
AMIN...
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...