Mkurungezi wa jiji la Mwanza, Bi. Dorothy Mwanyika akitoa nasaha zake kumuwakilisha mgeni rasmi Abbas Kandoro wakati wa uzinduzi wa benki ya CBA Mwanza. Mkuu wa Mkoa Kandoro alisisitiza umuhimu wa benki zote nchini kutoa mikopo kwa watu wote bila upendeleo.
Mkurungezi wa BOT jijini Mwanza, Bi. Edda Balele akizungumza na afisa mtendaji mkuu wa Benki ya CBA Mwl. Yohanne Kaduma wakati wa uzinduzi wa benki hilo tawi la Mwanza. Benki ya CBA imejizolea umaarufu nchini kutokana na mchango wake katika kusaidia sekta ya ujenzi nchini.
Mkurungezi wa BOT jiijini Mwanza, Bi. Edda Balele (kulia) akizungumza na mwenyekiti wa bodi ya benki ya CBA Bw. Ndewira Kitomari wakati wa uzinduzi wa tawi ya CBA Mwanza.
wafanya kazi wa benki ya CBA na wateja wa benki hio wakisikiliza kwa makini wakati wa uzinduzi wa tawi la benki hio Mwanza.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Jamani ni swali rahisi tu , kwani mkurugenzi kabwe aliyekuwa mwanza kaenda wapi sasa? nilikuwa sipo kitambo kidogo

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...