Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake wakati wa uzinduzi wa Kitabu cha ‘Quantum Mechanics’ kilichotungwa na Professa. John Kondoro, wakati wa hafla hiyo ya uzinduzi iliyofanyika leo Septemba 22, katika Ukumbi wa Chuo cha DIT, jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizindua rasmi Kitabu cha ‘Quantum Mechanics’ kilichotungwa na Professa. John Kondoro, wakati wa hafla hiyo ya uzinduzi iliyofanyika leo Septemba 22, katika Ukumbi wa Chuo cha DIT
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal (katikati) Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Prof. Makame Mbarawa (wapili kushoto) Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Charles Kitwanga (wapili kulia) Prof. John Kondoro mtunzi wa kitabu cha ‘Quantum Machenics’ na Makamu Mkuu wa Chuo cha DIT, Prof. Christian Nyahumwa (kushoto) wote kwa pamoja wakifurahia baada ya Makamu kuzindua kitabu hicho, wakati wa hafla hiyo iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Chuo cha DIT, jijini Dar es Salaam leo
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akionyesha kitabu cha ‘Quantum Machenics’ baada ya kuzindua kitabu hicho kilichotungwa na Prof. John Kondoro, wakati wa uzinduzi huo uliofanyika leo Septemba 22, katika Ukumbu wa Chuo cha DIT, jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi kitabu cha ‘Quantum Machenincs’ Makamu wa Chuo cha DIT, Prof. Christian Nyahumwa, ambao ni miongoni mwa watu wa kwanza kununua kitabu hicho kilichotungwa na Prof. John Kondoro, wakati wa uzinduzi wa kitabu hicho uliofanyika leo Septemba 22, katika Ukumbi wa Chuo cha DIT, jijini Dar es Salaam
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya maprofesa wa DIT baada ya uzinduzi wa kitabu cha ‘Quantum Mechanics’ kilichotungwa na Prof. John Kondoro. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
Sasa hapo Mh Bilali ndiyo umefika haswa kwenye fani yako ya mafizikia.
ReplyDeleteHongera Prof John Kandoro angalau watoto wetu watasoma kitabu kimeandikwa na mwenye jina la kibantu. Maprofesa wengine nanyi jitokezeni ili tupate vitabu vingi ambavyo waandishi wake ni wabantu.
WENZETU WAWEZE WANA NINI NASISI TUSHINDWE KWA NINI?
Hongera sana Prof Kondoro,pamoja na majukumu mengi umeweza kuandika kitabu ambacho sio tu kimekupa heshima kubwa bali kimeleta matumaini kwa watanzania waliokuwa na shauku kubwa ya kufaidika na utaalam wako katika fani hiyo, vile vile umeiletea DIT na wana DIT wote heshima kubwa.Kitabu hicho vile vile ni hazina kubwa ya kujivunia kwa kizazi cha leo na cha kesho.
ReplyDeleteAsante sana Profu. Kondoro kwa mchango wako wa elimu kwa taifa. Taifa letu linahitaji watu kama wewe. Hongera.
ReplyDeletethanx our prof.
ReplyDeletevp maprof. wengine,, nao wapo wapi,,?? au wanasubiria posho wakabanane na walio chini yao??
maana yake kuna maprof. tunabanana nao kwenye viposho hata elfu 10 mpaka ishirini kwenye madirisha ya malipo...LOL....