Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete leo amepokea hati za utambulisho kutoka kwa mabalozi wanne wanao ziwakilisha nchi hapa Tanzania.Walioziwasilisha hati zao leo ni pamoja na Balozi Luiz Javier Campuzano wa Mexico, Balozi Geoffrey Peter Tooth wa Australia,Balozi Sinnika Antila wa Finland na balozi Hossam Eldin Moharam wa Misri.Pichani balozi Bi. Sinikka Antila wa Finland akiwasilisha hati zake za utambulisho kwa Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete, ikulu jijini Dar es Salaam leo asubuhi


Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisaini kitabu cha maombolezo katika makazi ya balozi wa Cuba nchini Tanzania,Oysterbay jijini Dar es Salaam, kufuatia kifo cha Makamu wa Rais wa Cuba,Jenerali Julio Casa Regueiro.Aliyesimama Pembeni ya Rais ni Balozi wa Cuba nchini Tanzania Mhe.Ernesto Gomez Diaz(picha na Freddy Maro)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. kumbe adi ubalozi wa mexico upo bongo , hivi kwani kuna raia wengi wa mexico au cuba bongo , mtazamo wangu ni zinani kama kuna hao raia sana bongo. so ubalozi wa kama mexico una kazi gani bongo , kwani mimi najua sababu moja kubwa ya ubalozi kuwepo sehemu ni wengi wa raia wa nchi hiyo kuwepo kwa mfano wachina wapo bongo wengi pia wanafanya business trade sana na tanzania. je kuna huusiano gani kati ya mexico na tanzania?
    msaada kwenye tuta jamani kuusu hili jambo.
    mdau china

    ReplyDelete
  2. Poleni, rafiki wa kweli.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...