Serikali ya Kenya imesema licha ya changamoto za fedha, vifaa na wataalamu imejiandaa na kuweka mikakati ya kitaifa kukabiliana na maradhi yasiyo ya kuambukiza.
Kwa mujibu wa waziri wa afya wa nchi hiyo Bi Beth Mugo magonjwa kama saratani, kisukari, magonjwa ya moyo na matatizo ya kupumua ni magonjwa ya gharama kubwa kwa upande wa matibabu na wananchi, na serikali pekee hawawezi kukabilia bali mshikamano wa kimataifa unahitajika hasa katika kusaidia nchi masikini.
Akizungumza na mkuu wa idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa Flora Nducha waziri Mugo amesema pia tabia za watu kuhusu vyakula na maisha yao lazima zibadilike. Wasikilize.
(MAHOJIANO NA WAZIRI BETH MUGO)
http://www.unmultimedia.org/
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...