Mabalozi wanaowakilisha nchi zao kutoka nchi mbali mbali duniani kutoka Afrika,Ulaya,Asia,Marekani ya Kusini na Kaskazini na nchi za Ghuba  hapa Marekani,wamefika katika Ubalozi wa Tanzania(TANZANIA HOUSE) uliopo Washington,DC kujumuika katika kusaini kitabu cha maombolezo kufuatia msiba mkubwa ulilikumba Taifa la Tanzania kufuatia kuzama kwa meli ya MV Spice Islander katika mkondo wa Nungwi ,Zanzibar. Mabalozi hao kwa wingi wakiongozwa na mabalozi  kutoka Zimbabwe,Bahrain,Nicaragua,Namibia,Spain,Swaziland,Fiji, Spain,Mexico,Oman, Russia na kadhalika walionyesha kuguswa na ajali hiyo na kwa pamoja waliwaombea wahanga wa ajali hiyo na kuwaomba  wafiwa pamoja na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa na subira katika wakati huu huu mgumu kutokana na ajali hiyo mbaya katika historia ya usafiri wa majini visiwani Zanzibar.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. raia wa kawaida wa kitanzania wataruhusiwa lini ku sign hicho kitabu hebu tujulisheni jamani.mtanzania aishiye new york

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...