Mkuu wa mkoa wa Kagera aliemaliza muda wake (mstaafu),Mh. Mohamed Babu akimlaki Kanali mstaafu Fabian Massawe ambaye ni mkuu mpya wa Mkoa wa Kagera mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Bukoba, mkuu huyo wa mkoa aliwasili mkoani Kagera jana.

Mkuu wa Mkoa wa Kagera aliyeteuliwa na Rais Dkt. Jakaya Kikwete, kanali mstaafu Fabian Massawe akisalimiana na skauti mara baada ya kuvishwa skafu muda wakati wa kuwasili kwake mkoani humo kwenye uwanja wa ndege wa Bukoba.
Mkuu Mpya wa Mkoa wa Kagera,Kanali mstaafu Fabian Massawe akisalimiana na baadhi ya wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama wa mkoa wa Kagera.
Mkuu Mpya wa Mkoa wa Kagera,Kanali mstaafu Fabian Massawe akiwa amekumbatiana na mwenyetiki wa chama cha mapinduzi wa mkoa wa Kagera, Costancia Buhiye kwenye uwanja wa ndege wa Bukoba.
Mkuu mpya wa Mkoa wa Kagera, kanali mstaafu Fabian Massawe akisalimiana na ofisa wa TAKUKURU wa mkoa wa Kagera Domina Mkama.Picha na Audax Mutiganzi,Bukoba.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. yaani nyie hamnazo kweli,siamini kama tanzania inashindwa kuweka lami kwenye viwanja vya ndege vya mikoani.uzembe,ujinga,kukosa maarifa au ni nini maana ukiniambia swala la pesa nakataa,watu wanaunguza ma bilioni ya hela na mnajua hilo.

    ReplyDelete
  2. Bora huyu kaja kupokelewa na Toyota Noah aka mchomoko

    ReplyDelete
  3. masawe kala sana tangu jitegemee. DAh noma

    ReplyDelete
  4. hongera mzee masawe..you used to be my head master at jitegemee sec school....hongera sana!

    ReplyDelete
  5. jamani ukokagera akuna viogozi adi achagulie wa kutoka moshi.
    namkumbuka masawe alinichapa fimbo jitegemee asubuhi asubuhi kicha sikuchomekea , not fear at all, ilikuwa asubuhi nazani alitoka nyumbani kwake na asira zake akaona animalizie mimi! poa tu mungu upo!

    mdau USA

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...