Mtanzania anayecheza Soka ya kulipwa katika timu ya White Caps ya jijini Vancouver Canada,Nizar Khalfan akimkabidhi Rais Dkt. Jakaya Kikwete jezi ya timu yake wakati alipokwenda kumsalimu na kumshukuru kwa mengi aliyofanya katika kufufua na kuendeleza michezo na wachezaji Ikulu jijini Dar es Salaam leo jioni.(picha na Freddy Maro)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 17 mpaka sasa

  1. alikwenda kumtembelea na kumshukuru!...alikwenda kumshukuru nini?

    ReplyDelete
  2. Anamshukuru kwa kumleta Maximo wewe, bila Maximo watu wasingeonekana....

    ReplyDelete
  3. Jamani Ikulu ngoja na mimi nijipange kwenda, sasa sijui nitasema ninacheza mchezo upi!!! Lkn Mhe. amejitahidi sana kuwaweka wananchi wake karibu na Ikulu yao ila wanamichezo wamezidi. Kulikoni? Wachumi vipi?

    ReplyDelete
  4. good question and as they say thanks for nothing.a bunch of crap.

    ReplyDelete
  5. Kaenda kumchomea babu, anasema bora Maximo

    ReplyDelete
  6. Maamuzi magumu yanasubiri. Hivi mkuu wa Mkoa wa Dar ni nani?

    ReplyDelete
  7. Anamshukuru JK kwa kumleta Maximo na kumsaidia kuonekana...crap! Mi nadhani JK anapaswa kufanya ziara za mikoani sasa kuliko kushughulikia masuala ya namna hii. Nenda Shinyanga, Rukwa n.k. kakague miradi na kuwaeleza wananchi serikali yao itawasaidia vipi kukabiliana na njaa ya mwaka huu.

    ReplyDelete
  8. mimi nazani serekali wangefungua ka ikulu ndogo cha mikutano, ambayo raisi anaweza kukutana na yoyote hatakaye kwenda kumshukuru!
    mdau kenya

    ReplyDelete
  9. Ehe! nami ngoja nijipange kwenda ikulu....... labda mie niende kutazama siri za kuandika wiki leaks maana naona ni rahisi sana kuandika hata uwongo. Si nitajulikana nilikwenda ikulu?

    ReplyDelete
  10. Mnaotaka kwenda mjue kama unataka kwenda kujadili mada muhimu kama Kuepukana na mgao wa umeme , jinsi ya kufufua uchumi na kuongeza makusanyo ya kodi , na mengine yanayofanana na hayo mjue kabisa hamna nafasi

    ReplyDelete
  11. bado hamjakoma tu? hashim si mlimkaribisha hivyo hivyo? leo hii hayuko tena NBA (poor thang) sasa huyu kinachofuata nini?? chakula cha usiku? lakini ukiweka utani nyuma huyu kijana ni ana kipaji kweli, mi nilimwona anavyocheza, tuombe mungu tu atuletee KOMBE

    ReplyDelete
  12. kwanini hilo shati lisingekuwa na jina lake yeye mwenyewe mchezaji kama wachezaji wote wanavyofanya?? huyu kaka nani kamshauri hivyo? lakini ngoja tumpe muda labda atatujengea jina zuri huku canada

    ReplyDelete
  13. waswahili acheni majungu na wivu mtu basi asipate chansi huku ulaya?? ila tatizo wengi wakipata fursa ya kuwa chumba kimoja na JK wanajisahau basi hapo trip za bongo zitakuwa kila siku na ndio hapo atakapomalizikia, tuombe mungu huyu abakie huku kwa muda mpaka jina lake liote mizizi ndio awe anarudi rudi nyumbani kufanya vitu vyake.

    ReplyDelete
  14. KWA MAWAZO HAYO MLIYONAYO WATANZANIA KWA KWELI HATUTAENDELEA. KIONGOZI LAZIMA AWE KARIBU NA WATU WAKE. ALIENDA KUMSALIM RAIS NA KUMPA UZOEFU WA KIMICHEZO TOKA KWA WENZETU HUKO MAJUU. ACHENI SIASA JAMANI!

    ReplyDelete
  15. Uuuuuuiiiiiiiiiiii wajemeni hebu acheni wivu wakijinga.Kila kiongozi anastaili yake ya kuiongoza nchi.Anayo haki zote za kukaribisha mtu yeyote yule na kama ni kinyume na sheria basi nendeni mkamshitaki.Heeeee!!! mara mseme kazidi kukaribisha wananmichezo,mara kazidi kufutarisha mara sijui nini wacheni tabia zenu mbaya na roho za kwanini.

    ReplyDelete
  16. Kelele za sakafuni hazimkatazi mwenye Nyumba kulala. Semeni Semeni......hii nyimbo mnaijua. Kikwete hangoki mpaka 2015. Maandamano mbona hamkufanya. Slaa mbona kimya siku hizi au babu machokumchuzi kamweka plasta.

    ReplyDelete
  17. kwani mmeambiwa ikulu ni mbinguni watu hawawezi kwenda?

    Nawe unayesema aende mikoani hao wakuu wa mikoa na wilaya wanafanya kazi gani?

    Akiwa yuko Ikulu ooh safiri, akisafiri ooh Vasco da gama. kweli ubinadamu kaazi hasa ukiwa mbongo!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...