Tunawaarifu Watanzania wote wanaoishi na waliopo UAE kuwa kutakuwepo na Swala ya kuwaswalia Marehemu waliofariki kwenye ajali ya Meli ya MV Spice Islander huko Zanzibar.
Swalat Janaiz itafanyika siku ya Ijumaa baada ya SWALAT JUMAA kwenye MSIKITI WA ZANZIBAR RASHIDIYA.
Khitma ya Wanawake itakuwa baada ya SWALAT ASR hapohapo RASHIDIYA.
Khitma ya Wanaume itakuwa baada ya SWALAT ISHAA hapohapo RASHIDIYA.
Watanzania wote kutoka Falme zote za Abu Dhabi, Dubai, Sharja, Ajman, Umm Al Quwain, Ras Al Khaimah na Fujairah mnaombwa kuhudhuria.
Issa Majid Maggidi
Naibu KatibuJumuiya ya Watanzania UAE


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...