Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Posta Tanzania,Sabasaba Moshingi (kushoto) akikabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya sh. milioni 4 kwa Mbunge wa jimbo la Bukene mkoani Tabora,Mh. Selemani Zedi ikiwa ni msaada uliotolewa na benki hiyo kwa ajili ya kununulia madawati yatakayotumiwa na wanafunzi wa shule za msingi za jimbo hilo.makabidhiano hayo yamefanyika asubuhi hii katika ofisi ya makao makuu ya Benki hiyo,mtaa wa Samora jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Posta Tanzania,Sabasaba Moshingi akizungumza na vyombo vya habari mara baada ya kukabidhi msaada huo kwa Mbunge wa Jimbo la Bukene.
 Mbunge wa jimbo la Bukene mkoani Tabora,Mh. Selemani Zedi akitoa shukrani zake kwa uongozi wa Benki ya Posta Tanzania mara baada ya kupokea msaada wa sh. milioni 4 kwa ajili ya kununulia madawati yatakayo tumiwa na shule za msingi za jimboni kwake.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...