TAARIFA ILIYOIFIKIA GLOBU YA JAMII HIVI PUNDE,INAELEZA KWAMBA BASI LA DELUXE (PICHANI) LINALOFANYA SAFARI ZAKE KATI YA DODOMA NA DAR ES SALAAM,LIMETEKETEA KWA MOTO MAENEO YA KIBAHA KWA MATIUS MKOANI PWANI MARA BAADA YA KUPASUKA KWA TAIRI LA MBELE NA KUPELEKEA KUPASUKA KWA TENKI LA MAFUTA NA KUFANYA MLIPUKO.

AJALI HIYO IMETOKEA NUSU SAA ILIYOPITA KWA MUJIBU WA RIPOTA WETU ALIOPO ENEO LA TUKIO HIVI.

INASEMEKANA WATU 10 TU NDIO WALIOFANIKIWA KUTOKA KWENYE BASI HILO WAKIWA HAI LAKINI WENGINE WOTE WANASADIKIWA KUTEKETEA NA MOTO HUO.

GLOBU YA JAMII INAENDELEA KUFUATILIA KWA UKARIBU TUKIO HILO NA TUTAENDELEA KUTOA TAARIFA KADRI ZITAKAVYOKUWA ZINATUFIKIA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. mungu wasaidie ndg zetu waliopo ktk jali hiyo

    ReplyDelete
  2. mungu awalaze mahali pema waliopoteza maisha,na awape afya njema walionusurika

    ReplyDelete
  3. Its very bad,,alafu serikali inatangaza eti ni watu kumki tu wamepona,,si kweli

    Inasikitisha sana kwani hata waliokufa ni vigumu kuwatambua sura zao kwani miili yao imeharibika vibaya kwa kuungua na moto,,na sura zao hazitambuliki

    kikubwa ni tairi ya mbele kuw akipara,,na ain ay abasi yenyewe almaarufu kama UTONG haya ya kichina


    kwani mara bada ya mwereka (ups and down) lilibonyea paa,likashukua hivyo kupelekea dimension ya kioo kuwa ndogo hata ya kupitisha kichwa kwa ajili ya kujiokoa ( Haya mabasi bure kabisa) japo yanasifika kwamba hayana mabati ya kujeruhi watu lakini isue ni kwenye moto,,yamkini moto usingewaka wale ndugu zetu wangetoka wote

    Mimi kama niliyeshuhudia kw ambali bila kuw ana uwezo w akutoa mdaada wowote kwani moto ulikuw ani mkali mno,,hakuna aliyethubutu kusogelea imenisikitikitisha sana

    Ila kikubwa ni tairi ya mbele kuwa kipara na mwendo kasi n agari lililokuw ambele

    Ni hayo tu wadau wenzangu

    Mdau safarini kutoka Upareni

    ReplyDelete
  4. Imefika wakati Wakubwa walio madarakani hasa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ikafikiria kuwa na vituo vya zimamoto katika kila kitongoji hapa jijini na nje ya jiji. Hii ni kwa sababu mji umepanuka sana na wote tunategemea zimamoto itoke FIRE pale eneo la Jangwani Sekondari. Je hii ni haki kweli???

    Majanga yanaepukika na nadhani hata hapo Kibaha pia wanategemea magari yatoke Dar je hi halali?? Tupende maendeleo na tujiwekee mazingira ambayo yatatusaidia katika shida kama hii ya moto.

    Pole ndugu zetu mliopotelewa na ndugu katika ajali hii. Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema peponi. Na kwa walio hospitali tunawaombea wapone haraka.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...